Featured
Loading...

Wasichana kunigombania siyo dhambi – Steve Nyerere


Msanii mkongwe wa filamu Steve Nyerere amedai wasichana kugombana kwa ajili ya staa ni jambo la kawaida hivyo yeye ashangai kusikia bado kuna wasichana wanagombana kwa ajili yake.

Akiongea katika kipindi cha Uhondo cha EFM wiki hii, Steve Nyerere amedai ameshazoea kusikia wasichana wakigombana kwa ajili yake.

“Unapozungumzia kuna watu waligombana kwa ajili yangu, kwangu mimi kama staa inawezekana labda wameonyeshana kwenye picha, huyu ndo mpenzi wangu,” alisema Steve. “ Lakini unapokuwa super stars kuna watu wanampenda Will Smith yupo Marekani, kuna wabongo wanapigana kwa ajili ya Kim Kardashian. Kwa hiyo mimi nataka kusema inapofikia sehemu fulani ya mafanikio na watu wakakujua siyo dhambi kuongelewa, hata kwangu siyo dhambi, mimi napenda waendelee kuniongelea hivyo na kunipigania hivyo kwa maana ni staa,”

Mwigizaji huyo amesema kwa sasa anaishi na mwanamke na pia ana watoto.

Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )
© Copyright MZALENDO HURU
Back To Top