Mfanyabiashara
James Rugemalila anayekabiliwa na kesi ya utakatishaji fedha ameieleza
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa anahitaji kuonana na Mkurugenzi wa
Mashtaka nchini (DPP) ili ampe ushahidi wa nani anayepaswa kukamatwa
katika kesi hiyo.
December
8, 2017 Rugemarila aliieleza mahakama hiyo kuwa unahitajika ushirikiano
baina yake na upande wa mashtaka ili kumbaini mwizi wa Sh.Bil 309 za
Serikali.
Mbali
ya Rugemarila, Mshtakiwa mwingine ni mmiliki wa IPTL Harbinder Singh
Sethi ambapo kwa pamoja wanakabiliwa na mashtaka 12 ya uhujumu uchumi,
utakatisha fedha na kuisababishia Serikali hasara ya USD 22, 198,544.60
na Sh.Bil 309.
Rugemarila
ameyaeleza hayo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi baada ya
Mwendesha Mashtaka wa Takukuru, Leornad Swai kudai upelelezi wa kesi
hiyo haujakamilika, hivyo anaomba ahirisho.
Baada
ya kueleza hayo, Rugemarila alinyoosha mkono ambapo amesema kuwa
anaushukuru upande wa mashtaka ulimchukua gerezani na kumpeleka Upanga
kwa mahojiano na kumrudisha salama gerezani.
“Leo
nimekuja na ushahidi, hivyo naomba nikutane na DPP ili niweze kumsaidia
kumjua mwizi anayepaswa kukamatwa, kwani lengo letu ni kuonyesha kuwa
tupo Innocent,” alieleza Rugemarila.
Kutokana
na maelezo hayo, Hakimu Shaidi alimtaka Rugemarila kuwasiliana na
mawakili wake ili waandike barua ya kuwasilisha kwa DPP kuhusu suala
hilo la ushahidi wake, ambapo ameahirisha kesi hiyo hadi January 5,
2018.
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )