
Mbowe
amesema kuwa magari hayo yatafanya kazi pasipo kuwa na itikadi za chama
kwani wananchi wote ni wamoja hasa katika shughuli za kuleta maendeleo.
Amebainisha
kuwa gari moja lita tumika katika Hosipitali ya Wilaya ya Hai na gari
lingine lita tumika kutoa huduma katika hosipitali Machame ambayo
inamilikiwa na kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania.
Zifuatazo ni picha tofauti za tukio la kukabidhi magari hayo katika mkutano ulio fanyika Wilayani Hai eneo la Snoview Hotel.

Mbunge Freeman Mbowe akiwasili katika viwanja vya Snowview

Magari ya kubebea wagonjwa (ambulance)zikiwasili uwanjani

Mbunge Freeman Mbowe akiwa uwanjani hapo na kuonesha upendo kwa kumbeba Mtoto

Sehemu ya ndani ya gari la kwanza la kubebea wagonjwa.

Sehemu ya ndani ya gari la pili la kubebea wagonjwa.

Upande wa nyuma wa magari hayo kama unavyo someka.

Mbowe akikabidhi vitambulisho vya gari kwa Mkuu wa Jimbo la KKKT Jimbo la Hai
Mchungaji Asanterabi Swai
Mchungaji Asanterabi Swai

Mbowe akikabiti vitambulisho vya gari la kubebea wagonjwa kwa Mganga Mkuu wa
Hosipitali ya Wilaya ya Hai Dr Paul Chaote aliye pokea kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji.
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )