Featured
Loading...

Henry Kilewo:Dar es Salaam ipo Chini ya Chadema/Ukawa, Ndio Maana Analazimisha Serikali Kuhamia Dodoma


Nimesikia Mwenyekiti Mpya wa CCM Taifa ambaye alikuwa anagombea pekee ambaye pia alitangazwa na NEC kuwa Rais akisema atahamishia serikali yake Mkoani Dodoma kutoka Dar es salaam..
Ni kweli ni lazima serikali ihamie Dodoma kwakuwa Dar es salaam ipo chini ya Chadema/Ukawa na siyo CCM ndiyo maana analazimisha ihamie Dodoma.. Mkuu unasubiri nini? Ihamishie kesho maana Dar es salaam imewakataa ccm peleka sehemu ambayo Nec wamewatangaza...

Naelewa kuwa serikali kuhamia Dodoma ilikuwa ni adhima ya Mwl.Nyerere ila lilipouzwa kwakuwa Dar es salaam lilikuwa shamba la Bibi ila kwasasa kwakuwa Dar es salaam imeikataa CCM ni lazima Serikali ihamie Dodoma kama ambavyo imekuwa matakwa ya wengi na kupuuzwa... Tunakwenda kuichukua Dodoma 2020 na ndiyo mwisho wenu.....
Henry Kilewo
Katibu Greater Dsm (Chadema)

Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )
© Copyright MZALENDO HURU
Back To Top