Featured
Loading...

Msanii Mkongwe Ferooz Amalizwa na Madawa ya Kulevya....Mwenyewe Akana Kutumia


Msanii mkongwe wa bongo fleva aliyetamba miaka ya nyuma kidogo na nyimbo yake ya ‘Starehe’ iliyofanya vizuri sana amefunguka na kudai tuhuma zinazomkabili kuwa anatumia madawa ya kulevya sio za kweli hata kidogo.

Wasanii wengi waliokuwa wanafanya vizuri siku za nyuma huishia kuchukua njia mbaya na hivyo kuishia kujiingiza katika matendo maovu kama kuuza na kutumia madawa ya kulevya na hivyo kupelekea vipaji vyao kufa wengi wao hudai hujiingiza kwenye matumizi ya madawa ya kulevya kwa sababu ya ugumu kwenye gemu mfano wa wasanii waliojiingiza kwenye madawa ya kulevya ni pamoja na Ray C, Chiddi Benzi.

Ferooz ni moja Kati ya wasanii ambaye kwa kipindi kirefu ametuhumiwa kujihusisha na matumizi ya madawa ya Kulevya ambayo ndio yamepelekea kupotea katika ramani na kuzidi kuwa kimya tuhuma ambaxo Ferooz amezikana kwa nguvu shutuma hizo na kudai kuwa taarifa hizo hazifai kuaminiwa na watu wanaozisambaza ni wale wenye nia ya kumchafua na wasio mtakia mema.

Sijawahi kutumia dawa za kulevya na kama kuna mtu anayeshupalia kitu hicho tunaweza tukaweka dau tuende tukaangalie tuhakikishe na kama natumia sawa atakua ameshinda na jamii itakuwa imejua na kama nitaonekana situmii basi niondoke na dau langu na jamii itakuwa imeshajua situmii kitu kama hicho”.

Pia msanii huyo alielezea nia yake ya dhati ya kutaka kurudi kufanya muziki hivi karibuni kwa kutangaza kuwa anategemea kutoa ngoma yake hivi karibuni.

Shilawadu Mnaelekea Kaburini Kuna la Kujifunza Toka Kikundi cha ze Comedy ya Masanja


Miaka ya zamani kidogo Kikundi cha ZE COMEDY cha kina Masanja -mkandamizaji na wenzake kilikuwa na umaarufu na hata kupita baadhi wasanii wa muziki wa dansi, bongo fleva na hata bongo movies. Walikuwa wakipata mialiko mikubwa ya pesa ndefu kwenye sherehe, mikutano na majeshini kwenda kutumbuiza watu.


Kuna Kipindi Masanja alikuwa maarufu mpaka alikuwa hawezi kutembea mitaani hovyo bila ya walinzi na alijaribu hata kugombea ubunge katika jimbo moja huko nyanda za juu.Umaarufu wa ZE COMEDY ulianza kupungua baada ya kuanza kufanya vichekesho vya upande mmoja, kufurahisha wakubwa, kulewa sifa na kujiingiza kwenye siasa au kukubali kutumiwa na wanasiasa.

KIPINDI CHAO CHA SAA MOJA USIKU ENZI HIZO KILIKUWA MAARUFU KULIKO HATA TAARIFA YA HABARI.

Kipindi cha SHILAWADU ingawa nao walianza kwa kasi lakini naona wanaanza kuelekea kaburini.Kama SHILAWADU ni kuhusu umbea ni kwanini umbea mwingine wanaogopa kusema ,kwaninini siku hizi kila umbea wanaosema wa msanii unafuatana na kutambulisha wimbo mpya wa msanii, ina maana sio umbeya tena ni vitu mnapanga kabla, matangazo yamekuwa mengi na mmebakiwa na vitu viwili tu ni HAMISA MOBETO na DIAMOND.

Hata leo najua MAPOVU NI HAYO TU na mtakuwa mnaandaa msanii wa kutambulisha ngoma mpya baada ya kutunga skendo, hivi ile ya zamaradi na Ruge mbona ahtukusikia mapovu!!!

KUWENI MAKINI mnaelekea kubaya

By Kasulamkombe

RIWAYA: She is My Wife- Sehemu ya 29 & 30

MWANDISHI : EDDAZARIA

ILIPOISHIA
Mtu huyo wa ajaba akaendelelea kutazama tazama kila kona ya sable hii, akapiha hatua mbili mbele na kuzama ndani kabisa ya sable hii, na kuwapa mgongo Rahab na Raisi Praygod walio simama nyuma yake. Akaendelea kuvuta vuta pumzi, iliyo muashiria kwamba humu ndani kuna binadamu waklio hai, akalikoki bunduli lake aina ya gobore na kulishika vizuri huku kidole chake kimoja akiwa amekizamisha kwenye traiga, kwa haraka  akageuka nyuma na kuwaona Rahab na Raisi Praygod wakiwa nyuma yake wanamtazama

ENDELEA
Kwa haraka Rahab akaruka hewani na kuipiga teke bunduki ya mtu huyu mwenye muonekano wa ajabu sana, bunduki yake ikaanguka chini na kumpa nafasi nzuri Raisi Praygod kumrukia mtu huyo kwa kutumia bega lake lililo tua begani kwa mtu huyo na wote wawili wakaanguka chini.

 Rahab kwa haraka akaiokota bunduki ya mtu huto na kwakutymia kitako cha bunduki hiyo aina ya gobore akampiga nayo kichwani zaidi ya mara kumi mtu huyo, na kupelekea kichwa cha mtu huyo kupasuka kwa na kuvuja damu yenye rangi nyeusi ti.
“Mtu gani huyu….?”
Rahabu aliuliza huku akihema kwa nguvu akionekana kuchanganyikiwa kwa kumuona mtu wa aina hii ambaye tangu azaliwe hajawahi kumuona.

“Tuondike hakuna haja ya kuendelea kukaa hapa”
Raisi Pragod alizungumza huku akichungulia mlangoni kutazama kama wale watu wengine wa kutisha wamesha ingia ndani walipo kua wakiingiza mizoga ya watu walio waua. Wakatoka nje wakiwa katika tahadhari kubwa huku Rahab aklwa ameishika bunduki ya mtu huyo.

Wakafanikiwa kutoka nje pasipo kuonekana na watu hao ambao wapo ndani ya kijumba chao wakiendelea kuwakata kata vipande marehemu walio wachukua na kuwafanya ndio chakula chao cha usiku. Wakaanza kutokomea porini huku wakimuomba Mungu waweze kutoka kwenye msitu huu ambao bado haujawapa matumaini ya kuweza kuziokoa nafsi zao zilizo kwenye matatizo makubwa

Hasili ya watu hawa wa kutisha wanajulikana kama Mazombi, walio anza kujitokeza mwaka 1819 katika bara la ulaya. Inasemekana watu hawa ni wale walio weza kupoteza maisha kwa sumu zenye kemikali kubwa na waliweza kurudi katika ulimwengu huu wakiwa katika hali hiyo ya kutisha na kuweza kuwafanya wanadamu halisi kama ndio vitoweo vyao vya kila siku.

Rahab na Raisi Praygod wakaendelea kukata mbuga pasipo kuchoka, japo wanatamani kuweza kupata japo dakika waweze kupumzika, ila kila walipo kumbuka maiti za watu walio waona wakishushwa na mazombi hayo hawakutamani kamwe kuweza kusimama.

Hali ya majonzi ikawatawala mazombi walio mshuhudia mwenzoa aliye pasuliwa kichwa na kusababisha ubongo wote kumwagika nje. Hawakua na hamu hata ya kuendelea kupata vitoweo walivyo kuja navyo na ziadi kila mmoja akachukua silaha yake na kuingia msituni kufwatilia watu hao walio sababisha mauaji ya mmoja wao. Kutokana na kuufahamu vizuri msitu wao, wakajigawa kwenye makundi ya mazombi wawili wawili na kupelekea kuwa na vikundi vinne. Kila mmoaja akajiapiza kuweza kufanya mauaji ya kikatili kwa watu walio sababisha mauji ya mpendwa wao
                                                                                                    ***
Samson na wezake wakafanikiwa kufika katika kiswa cha Kunashir nchini Russia, kwa bahati nzuri wakafanikiwa kupokelewa na mkuu wa kikiso kilicho asi nchi ya Russia bwana Rusev, Wakapelekwa moja moja kwa moja kwenye jengo lenye ofisi za kikundi hichi kinacho endelea kufanya mapinduzi kwenye nchi yake ikiitaka serikali kuweza kuunda serikali mbili, ili wao  wajipatie mamlaka ya kuweza kutengeneza silaha hatari za nyuklia.

Kila mmoja akakabidhiwa kinywaji alicho kihitaji yeye, ili kuweza kujipozwa kwa uchovu mwingi wa safari yao ndani ya maji, tangu pale walipo kamtwa na jeshi la polisi nchini Tanzania. Fetty na wezake hawakuwa na uwezo wa kuielewa lugha ya kirusi, ambayo Samson yeye aliweza kuizungumza vizuri pasipo matatizo ya aina yoyote. Alicho kua akikifanya Samson ni kuwatafsiria kila kitu ambacho alicho kua akikizungumza na bwana Rusev.

“Jamaa anauliza eti, tunaweza kujiunga na kundi lake?”
“Mmmm……!!” Anna aliguna
“Hatuwezi sisi tupo hapa kwa ajili ya biashara”
Samson akamjibu bwana Rusev kitu alicho kizungumza Fetty anaye onekana kuto kubaliana na swala zima la wao kujiunga na kundi la bwana Rusev
“Je anauliza tunahitaji kiasi gani cha pesa ili tuweze kumkabidhi hii manohari?”
“Sasa hapo ndio umenena la maana” Halima alizungumza huku akitabasamu
“Anatulipa kwa dola au shilingi?” Agnes aliulza
“Hembu na wewe acha ushamba wako, huku shilingi aitolee wapi?” Fetty alimkosoa mwenzake
“Haya yaishe kiongozi Fetty”
“Muambia sisi tunataka dola milioni mia zinatutosha”
Samson akamgeukia bwana Rusev na kumueleza kiasi walicho kitaja wezake na bwana Rusev hakuwa na hiyana zaidi ya kukubali kuwalipa kiasi hicho.

RIWAYA: She is My Wife- Sehemu ya 25 & 26


MWANDISHI : EDDAZARIA

ILIPOISHIA....
“Raisi……!!”
Rahab alizungumza baada kwa mshangao baada ya kutokumuona Raisi Praygod kwenye usawa wa bahari jambo lililoanza kumpa wasiwasi mwngi.Ikamlazimu kurudi tena ndani ya maji, kutazama kama anaweza kumuona raisi, ila hakumuuona
“Mungu wangu!!”
Rahabu alizungumza kwa kuhamaki baada ya kuona kitu kikija kwa kasi katika upande aliopo yeye, kwa haraka haraka akagundua kwamba ni samaki mmoja hatari aina ya Papa, ndiye anaye karibia kufika katika eneo alilopo.

ENDELEA.....
Rahab akaanza kujipapasa mwiki mwake kwa haraka, kwabahati nzuri akakikuta kisu kwenye mguu wake wa kulika katika sehemu ya kiatu alipo kichomeka kipindi alipokuwa akivaa, nguo alizo nazo kwenye chumba maalmumu cha kuhifadhia nguo katika ndege ya raisi iliyo anguka muda mchache uliopita.

Akajiweka tayari kwa kupapambana na samaki huyu anaye mfwata kwa kasi katika eneo ambalo  ameangukia, kufumba na kufumbua samaki huyu tayari akawa aweshafika katika eneo alipo Rahab, kwa ustadi wa hali ya juu Rahab akajigeuza ndani ya maji na kushuka kwa kasi ndani ya maji, na kusababisha samaki huyu mkubwa kupita juu yake, kwa kasi jambo lililo zidisha ukali wa samaki huyu mwenye uchu wa kutafuna kiumbe chochote kitakacho ingia kwenye enoa la bahari alipo yeye

Rahab akakishika vizuri kishu chake chenye ncha kali, na kutazama jinsi samaki huyu anavyo kunja kona na kurudi katika eneo alipo kwa kasi kubwa, samaki akamfikia Rahab kwa karibu kabla samaki hajafanya maamuzi ya aina yoyote, Rahab akamuwahi kumchoma kisu kwenye eneo la tumbo la samaki huyu, lenye ngozi laini na kuanza kulichana kwa kutumia nguvu nyingi, jambo lililo sababisa damu nyingi kutapakaa katika enoa la sehemu walipo, huku utumbo mwingi wasamaki huyu ukitapakaa kwenye maji
“Haaaaaaaa”

Rahab alizungumza huku akichomoza kichwa chake kwenye maji, huku akivuta pumzi kwa wingi, akajilegeza mwili wake na kuufanya uanze kuelea elea juu ya maji, huku akitazma juu mwili wake ukiwa umechoka sana
                                                                                                  Agnes akamgeuza mtu aliye anguka na kumchunguza vizuri na kugundua kwamba anamajeraha kadhaa kwenye mwili wake, Agnes akapiga mluzi ulio mfikia Halima aliyekuwa katika eneo la karibu, Halima akapa hatua za haraka hadi katika sehemu alipo simama Agnes
“Best kuna mtu hapa nimemuona”

Agnes alizungumza huku akimgeuza mtu aliye lala chini huku damu zikimvuja, Halima akamtazama mtu aliye lala chini kwa umakini, pasipo kuzungumza kita cha aina yoyote, kiasha akaikoki bastola yake akiziweka risasi zilizopo kwenye magazine yake, kuwa tayari kutoka nje, kitu kikubwa alicho kibakisha ni kuivuta traiga ya bastola yeka kuziruhusu risasi atakazo zihitaji kutoka nje

“Halima unataka kufanya nini?”
“Hastahili kuishi, mtu mwenye ni mfu huyu”
“Hembu ngoja kwanza?”
“Nini?”
“Usimuue?”
“Sasa anabaki duniani wa kazi gani, unamtambua huyu mtu”
Halima alizumgumza kwasauti iliyo jaa msisitizo mwingi
“Hata kama, simfahamu ila kuna kitu ninacho kihisi kwa huyu jamaa”

“Kwanza ametokea wapi?”
“Mimi sifahamu, ila nilisikia kishindo, nilipo kuja hapa ndipo nilipo muona huyu jaamaa akiwa amelala hapa”
Halima pasipo kuuuliza akafyatua baadhi ya risasi, jambo lililo muudhi sana Agnes na kumfanya amsukume Halima na kuangukia pembeni

“Mbona unakuwa mpumbavu wewe, nini unafanya”
Agnes alizungumza kwa hasira huku akimfokea kwa nguvu Halima aliye angukia pembeni, kwa bahati nzuri risasi alizo zifyatua Halima alizipiga pembeni ulipo mwili wa jamaa na hapakuwa na risasi iliyo ingia katika mwili wa mtu waliye muona.

Milio ya risasi ikawastua Fetty pamoja Anna ikawalazimu kutoka nje ya ‘submarine’ na kuelekea sehemu walipo isikia milio ya risasi huku wakiwa makini sana, kila mmoja akiwa ameishika bastola yake mkononi, waakawakuta Agnes na Halima wakiwa wanafokeana huku kila mmoja akionekana kuwa na jazba ya ajabu, Fetty akafyatua risasi mbili hewani nakuwafanya  Agnes na Halima kunyamaza
“Nyingi mumechanganyikiwa?”
Fetty aliuliza kwa sauti juu huku akiwatazama Halima na Agnes

RIWAYA: She is My Wife- Sehemu ya 19 & 20


MWANDISHI : EDDAZARIA G.MSULWA

ILIPOISHIA...
“NDUGU ABIRIA, NIFURAHA YANGU KUWA NANYI KATIKA SAFARI HII, NIMETOA LISAA MOJA KWA KILA ABIRIA KUSALI SALA YAKE YA MWISHO KWANI NDEGE INAKWENDA KULIPUKA NDANI YA LISAA HILO KUTIMIA KAMA HUAMINI, TIZAMA HII”

Samson akaishika camera na kuigeuzia kwenye computer aliyo iietega mwendo kasi wa saa, unao onyesha dakika zake zikirudi nyuma, kwani ikifika ndani ya muda alio upanga, mfumo mzima wa ndege unakwenda kuzima, na litakalo tokea hapo ni ndege kulipuka, jambo lililo anza kumuogopesha kila mmoja aliyomo ndani ya ndege hadi raisi mwenyewe

ENDELEA...
Samson akaigeuzia kamera alipo na kuznedelea kuzungumza kwa sauti iliyo jaa msisitizo
“NAJUA MUTASHANGAA, ILA NI KWAMBA NITAHITAJI RAISI KUFANYA HAYA YOTE AMBAYO NITAMUAGIZA KUFANYA LA SIVYO PUUUUUUU, SOTE TUTAKUFA HAHAHAAAAA”
Samson akaanza kucheka kicheko kilicho muacha mdomo wazi Rahab ambaye hadi sasa hivi amuelewi Samson anamalengo gani na roho yake

Fetty, Anna, Agnes na Halima hawatambui ni wapi wanapo elekea, kila mmoja akabaki akiwa na wasiwasi moyoni mwake kwani, nyuso zao bado zimefunikwa na vitu mifuko mnyeusi, isiyo wapa uwezi wa kuona kinacho endelea zaidi ya pumzi zinazo ingia kwenye pua zao.Kila mmoja anahofu ya kuuliza ni wapi wanakwenda kutokana kila jibu walilo pewa apo awali ni kwamba wanaelekea kuzimu.Wakasikia mlango wa chuma ukifunguliwa kwenye chumba walichopo.
“Yupi mkuu”

Sauti ya mwanaume ilisikika kwenye masikio yao, na hawakujua ni nani anaye uliziwa
“Huyu mwenye mahipsi makubwa”
Mkuu wa askari alijibu kupitia redia ya upepo, huku akitazama kwenye moja ya Tv iiyopo kwenye chumba chake, ikionyesha video za kamera za ulinzi zilizopo kwenye chumba walichopo Fetty na wezake

“Ahaa sawa mkuu”
Askari aliye agizwa na mkuu wake wa kikosi, akamkamata Anna, na kumnyanyua juu
“Jamani munanipeleka wapi?”
Anna alizungumza huku akijitahidi kujitoa mikononi mwa askari huyo
“Tulia wewe, nitakuua malaya mkubwa wewe”
Askari huyo akamnyanyua Anna na kumuweka begani mwake, na kutoka kwenye chumba na kuuamiza mlango kwa nguvu
“Hakikisheni hatoki mtu hapa”

Askari huyo aliwaagiza askari wengine wawili, walio simama kwenye malango wakilinda chumba walichopo majambazi hawa wa kike.Askari aakendelea kumbeba Anna ambaye anaendelea kufurukuta kwenye bega lake alipo muweka, kutokana na ukubwa wa misuli yake iliyo jengeka vizuri kutokana na mazoezi ya kijeshi anayo yafanya, Anna hakumsumbua kabisa kuchomoka kwenye mikono yake.Wakafika kwenye moja ya chumba ambacho yupo mkuu wake wa kikosi bwana Mathiasi Reymond na kumuingiza Anna na kumkalisha kwenye kiti
“Tulia kama ulivyo la sivyo tutakunyonga”

Anna aliendelea kupokea vitisho kutoka kwa askari aliye mtoa kwenye chumba alicho kuwepo na wezake.Mathiasi Reymond, tayari amesha vua ngua zake na kubaki na bukta yake ya ndani kwa ajili ya kufanya kazi moja tu, yakumuingilia kimwili Anna, msichana mzuri aliye umbika kila idara ya mwili wake.

Fetty akanyanyuka kwenye kwenye sehemu aliyo kaa, lengo lake ni kusikiliza kama atapokea amri yoyote ya kuambiwa kukaa kwenye sehemu yake, ila ukimya ukatawala.Akapiga hatua za taratibu akizunguka kwenye chumba akijaribu kujua ni kitu gani kinacho endela ila hakusikia chochote.

“Jamani mupo”
Fetty alizungumza kwa sauti ya chini
“Ndio, ila tupo wa tatu”
Halima alijibu kwa sauti ya kunong’oneza
“Nalijua hilo, Anna atakuwa amepelekwa wapi?”
“Yaani hata mimi mwenyewe sielewi?” Agnes alijibu
“Sijui hapa ni wapi jamani” Agens aliiuliza
“Cha msingi ni kujua nini tunatakiwa kukifanya na amini mumenielewa”

Fetty alizungumza huku akijiegemeza kwenye ukuta wa chumba alichopo, kutokana na mikono yake kufungwa kwa nyuma kwa pingu na kugundua si ukuta wa kawaida

Mathiasi Reymond akamuamuru mlizi wake, kumfungua  vipingu za mikononi na minyororo aliyo fungwa Anna kwenye miguu yake na mlinzi wake akafanya kama alivyo agizwa na bosi wake.Baada ya mlinzi wake kumfungua Anna akatoka ndani ya chamba na kumuacha bosi wake na Anna
                                                                                            
Vichwa vya viongozi wa pande zote mbili Tanzania na Marekani vinazidi kuuma, kila mmoja akijaribu kutafuta mbinu na njia za kuweza kuipata ndege yenye thamanini sana aina ya Air Force inayomilikiwa na serikali ya nchini Tanzania huku ndani mwake ikiwa imembeba raisi pamoja na viongozi wapambe wake.Juhudi za Satelait katika kuinasa ndege ya raisi na kutambua ni wapi ilipo inafua dafu, jambo linalo zidi kuwachanganya sana viongozi wa pende zote mbili.

Wanacho kihofia viongozi wa nchini Tanzania ni kumpoteza raisi wao mpendwa bwana Praygod Makuya, huku serikali ya Marekani ikihofia kupoteza moja ya ndege zake ambazo ina uwezo mkubwa wa kuhimili mikiki mikiki ya vita ya anga japo imetengenezwa kistarehe zaidi kwa ajili ya kumbeba raisi huyu wa Tanzania aliye jijengea umaarufu mkubwa sana kutokana na ucheshi wake na ushirikiano wake kwa wananchi na vingozi mbali mbali duniani, katika mataifa tajiri na mataifa masikini

“Inatuazimu kutumia, mpango namba mbili(Plan B)”
Mkuu wa jeshi la anga alizungumza na mkuu wa jeshi la anga nchini Tanzania kwa kupitia mtandao wa kuonana moja kwa moja katika vioo vya Tv zao kubwa zilizopo kwenye maofisi yao ya jeshi.

RIWAYA: She is My Wife- Sehemu ya 17 & 18

 

MWANDISHI : EDDAZARIA G.MSULWA

ILIPOISHIA...
Samson alizungumza kwa sauti ya ukali, huku akimtumbulia mimacho Rahab
“Unaniuliza wewe kama nani?”
“Sio ninakuuliza kama nani, ila nataka kujua unataoka wapi kumbuka kwamba hapa upo kwangu?”
“Hupaswi kujua, mwehu nini wewe?”
Samson akanyanyuka kwa hasira na kumzaba Rahab kibao cha shavuni kilicho myumbisha hadi kikamuangusha chini

ENDELEA...
Rahab akasimama kwa hasira, akarusha ngumi ambayo Samson aliidaka kwa mkono wake mmoja na kuachia kibaoa kingine kizoto kilicho myumbisha Rahaba na kumuangusha chini.
“Sikiliza wewe mwanamke, hata siku mmoja huto weza kunipiga sawa”
Samson alizungumza kwa kujiamini huku akimtazama Rahab anaye jifikiria kunyanyuka kutoka katika sehemu aliyo angukia.Rahba akarusha teke akikusudia kuipiga miguu ya Samson, ila Samsona akaruka juu na kutua chini, akamnyanyua Rahab kwa mkono mmoja na kumvuta karibu yake
“Nitakuumiza”

Rahab akajaribu kumpiga Samson igoti cha tumbo ila Samson akawahi kurudi nyuma, huku akimsukumiza  nyuma Rahab.Rahab kwa hasira akarusha teke, akiwa hewani Samson akamuwahi kwa kupiga tele la mbavu lililo sababisha Rahab kuangukia kitandani huku akihema
“Usijaribu tena siku nyingine”

Samson alizungumza huku akimtazama Rahab anaye ugulia maumivu ya mbavu zake.Rahab akamtazama Samson kwa jicho kali lililo jaa maswali na mashaka mengi juu ya Samson kwani kwa jinsi alivyokuwa anamchukulia sivyo jinsi Samson alivyo

“Wewe ni nani?” Rahab aliuliza
“Mimi ni Samson, au unahisi mimi ni nani?”
“Ninamaanisha unafanya kazi gani?”
“Haaaa mimi si fundi baiskeli”

Samson akafungua boksi lake la kuhifadhia nguo zake, akatoa bastola mbili na kumkabidhi Rahab,
“Nenda kafanye kazi yako kwa umakini”
Samson alizungumza huku akijilaza pembeni ya Rahab, huku akijifungua vifungo vya shati lake.Rahab akaichunguza moja ya bastola zake na kuikuta ikiwa na risasi za kutosha, kwa haraka akajigeuza na kumkala tumboni Samson na kumuweka bastola ya kichwa.
“Sema wewe ni nani?”

Rahab alizungumza huku jasho jingi likimwagika, Samsona akamtazama kwa umakini Rahab kisha akaunyanyua mkono wake wa kushoto pasipo kuwa na waga na kuushika mkono  wa Rahab alio shika bastola yake na kuusogeza pembeni, mkono wa kulia wa Samson ukapakishika kiuno cha Rahab na kumvuta chini taratibu na sura zao zikawa zimesogeleana kwa ukaribu sana
“Mimi ni fundi baiskeli”

Samson alizungumza kwa sauti ya upole iliyo jaa hisia nyingi za mapenzi, kisha taratibu akaukutanisha mdomo waka nawa Rahab, na kuanza kubadilishaa ladha ya mate yao, kila mmoja akajikuta mwili wake ukisisimka kwa kiasi cha kuzidi kuziinua hisia zao za mapenzi huku kila mmoja akijitahidi kumnyonya mwenzake vilivyo, wakaanza kuvuana nguo moja baada ya nyingine na kujikuta wakizama katika dimbwi kubwa la mapenzi, huku kila mmoja akionekana kuwa na furaha ya kupata penzi la mwenzake
                                                                                         
Ndege maalumu ya jeshi ikawekwa tayari kwa safari ya kuwasafirisha Fetty, Halima, Anna na Agnes, ambao tangu wakamatwe maisha yao yamekuwa ni yakufungwa vitambaa vyeusi machoni, huku mikononi na miguuni wakiwa wamefungwa cheni nzzito ambazo si rahisi kwa wao kuweza kuzifungua.Wakavalishwa mavazi ya rangi ya chungwa, yanayo endana na mavazi ya mafundi gereji wengi.Safari ikapangwa kuondoka nchini usiku wa saa nne

Waandishi wa habar pamoja na wananchi wenye hasira kali na wasichana hawa, wamejipanga pembezoni mwa barabara wakisubiria kuwaona wasichana hao wakipelekwa katika uwanja wa ndege kwa ajili ya kuanza safari ya kupelekwa mahakama kuu ya magaidi.Kila mmoja moyoni mwake akawa na sala kubwa ya kuomba wahukumiwe kifungo cha maisha kwani ukatili ambao wameufanya ni mkubwa, ambao haukuwahi kutokea katika nchi inayosifika kwamba ni nchi ya amani.

Kikosi maalumu cha wanajeshi wapatao ishirini na tano, wakiwa na bunduki zao mikononi, wamesimama nje ya magari kumi aina ya GVC yanayotumiwa kusafirishia wahalifu harari, Sifa ta magari haya ni kwamba hayaingii risasi na yametengeneza kwa uwezo mkubwa wa kuhimiili mikiki mikiki ya majambazi endapo wanaweza kuvamia msafara wao.Nitukio la kihistoria nchini Tanzania kwani haijawahi kutokea ndio maana watu wengi pamoja na waandishi wa habari wanaamu ya kushuhudia jinsi msafara huo utakavyokuwa na ulinzi mkali kupita misafara yote ya magaidi walio wahi kukamatwa na jeshi la polisi

Magari yote kumi yakawa yapo tayari kwa safari, wanajeshi hao wakiwa wanasubiria kuletwa kwa magaidi hao walio chini ya ulinzi mkali wa askari.Simu ya IGP Bwana G.Nyangoi inata zikiwa zimesalia dakika tano tu kabla hawajawafungulia magaidi kutoka kwenye chumba maalimu kilicho tengenezwa kwa kuta za chuma, na  kuwakabidhi katika kikosi maalumu cha jeshi

“Ndio mkuu” Bwana Nyangoi alizungumza baada ya kuipokea simu yake
“Wahalifu , wabadilishieni msafara”
“Muheshimiwa mbona kila kitu tumeshakiweka kwenye utaratibu”
“Hii ni amri na sio ombi, wasafirisheni na sabmarine”
                                                                       
Rahab na Samson, wakiwa wamevalia nguo za wahudumu wa ndege ya raisi aina ya Air Force, wanafnikiwa kuingia katika ndege, pasipo kustukiwa huku Samson akiwa ametengeneza vitambulisho bandia vinavyo endana na wahudumu kwenye ndege ya Raisi wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Dokta Praygod MakuyaMbaya zaidi katika siku hii, mtaalamu anaye kagua watu wanao ingia kwenye ndege ya raisi kwa kutumia mashine maalumu, anaumwa sana kiasi kwamba ameshindwa kuwemo katika ndege hii ya raisi, na watu wengine hawana utaalamu wa kuitumia mashine hii kutoka ndege ni mpya katika maisha yao.Samson katika mfuko wake wa nyuma wa suruali ameweka kipakti kidogo chenye madawa ya kulevya yenye nguvu kubwa ya kumlewesha mtu katika muda wa dakika tano tuu

Watu wengi wamezoea kumuona Samson kama fundi baiskeli, na ndivyo jinsi watu wengi wanavyo aminni katika hilo, ila sivyo kama watu wengi wanavyo dhania.Samson ni miongoni mwa wapelelezi wa hatari kutoka nchini Somalia katika kundi la Al-Shabab, Wazazi wake ambao kwa sasa ni marehemu ni watanzania na ameishi Tanzani tangu akiwa mtoto mdogo na kupata elimu yake ya msingi katika shule ya St. Mary, ila alipo timiza umri wa miaka kumi na mbili aliwashuhudia wazizi wake, baba na mama wakiuwa kinyama na Bwana Praygod Makuya ambaye kwa kipindi hicho alikuwa ni waziri wa mambo ya nje, wazazi wake walikuwa ni walikuwa ni miongoni mwa wanasiasa mashuhuri nchini Tanzania kutoka katika chama pinzani, kinachokichua chama kilichopo madarakani katika nafasi za kugombania madaraka ya uraisi.

RIWAYA: Sorry Madam - Sehemu ya 59 & 60 (Riwaya inawafaa kuanzia miaka 18 na kuendelea )


 Mtunzi : Eddazaria g.Msulwa


Ilioishia...
Hadi kunapambazuka sikuweza kumuona nesi phidaya, hali ya hatari ikaanza kunijia kichwani mwangu na kuhisi nesi phidaya anaweza kuwa amekutwa na matatizo, mlango ukafunguliwa na wakaingia manesi wawili pamoja na madaktari wale wawili.Wakaanza kufungua kitandana na kukishusha chini kidogo hadi kikafikia usawa mzuri wa kuweza kusukumwa.Pasipo hata ya kunisemesha wakaanza kunisukuma na kunipeleka nisipo pajua huku nyuso zao zikiwa na tabasamu ambalo sikuliewewa nini maana yeke

Endelea...
Wakazidi kukisukuma kitanda nilicho lalia hadi hadi tukafika kwenye maja ya mlango ambao juu kuna maandishi ya kiharabu ambayo sikuweza kuyaelewa, nesi mmoja akausukuma mlango na kufunguka, na wakaniingiza ndani nikiwa juu ya kitanda changu, mwanga mwekundu wa taa ulioo ndani ya chumba ukazidi kuniogoesha.Chumba kizime kimezungukwa na mashine mbalimbali ambazo sikujua zinakazi gani.Daktari mmoja akachukua mashine yenye kimviringo mbele, kisha akakiwasha na kuanza kuzunguka, akachukua moja ya miwani kubwa ambayo ni nyeupe akaivaa na kuanza kucheka kitu kilichoo zidi kuniogopesha zaidi.

Gafla taa ya mwanga mweue ikawashwa na kuwafanya madaktari na manesi, kustuka, macho yetu wote tukayaelekezea mlangoni na kumuona nesi phidaya akiwa ameshika, bastola huku jasho jingi likiwa linamwagika usoni, akaanza kuzungumza kwa kiarabu na taratibu madaktari wakanyoosha mikono juu wakitetemeka, akazungumza neno lililo wafanya  madaktari kuanza kurudi nyuma kutoka kilio kitanda changu.
“eddy, wamekufanya chochote kibaya?”
“hapana”
“powa”

Nesi phidaya akazungumza neno jengine lililowafanya madaktari na manesi kulala chini, sakafuni huku mikono yao wakiwa wameiweka juu ya vichwa vyao.Nesi phidaya akanifwata hadi kitandani na kuuitisha mkono wake mmoja kwenye, mgongo wangu na kuniomba niwe kushuka chini, japo ninajihisi maumivu ila nikajikaza kiume kwani kuendelea kukaa haoa kutahatarisha maisha yangu.
“jikaze baba yangu”

Nesi phidaya alizungumza huku akiendelea kunishusha kwenye kitanda, akanisaidia kusimama vizuri, huku muhimili wangu wote wa kusimama nikiutegemea kutoka kwake, nesi phidaya akawatazama watu madaktari walio lala chini, akazungumza neno la ukali lililo wafanya madaktari na manesi kuzidi kuzifunika sura zao chini pasipo kuzinyanyua juu.Tukafanikiwa kotoka nje ya chumba walicho niingiza, nesi phidaya akafunga mlango kwa nje na sote tukaanza kuondoka taratibu huku nesi phidaya akiificha bastola yake na baadhi ya wahudumu wakabaki wakiwa wanatushangaa.Tukatoka nje na kukuta gari aina ya taksi ikiwa inatusubiria

“ahaaaa”
Nilitoa mguno wa maumivu baada ya mguu wangu nilio vunjika kugongwa kwenye mlango nilipokuwa ninajiaandaa kuingia ndani ya gari, siti ya nyuma
“pole eddy”
“asante”

Nesi phidaya akanisaidia kuingia ndani ya gari na kufunga, kisha yeye akaingia kwenye siti ya mbele kwa dereva na kumuongelesha dereva kiarabu na akaliondoa gari lake kwa kasi.
“asante sana, nesi phidaya”
“usijali nipo kwa ajili yako, ila ningependa uniite phidaya tu na si nesi phidaya”
“sawa”

Nikaendelea kujilaza kwenye siti ya nyuma ya taksi tuiyo ipanda, ila kuna mwanga mkali wa taa ukawa unaingia kwenye gari letu, ikanilazima kunyanyua kichwa changu kutazama nyuma, nikaona gari ndogo ikija kwa kasi sana,
“phidaya kuna watu wanatufwata nyu……”

Kabla sijamalizia sentesi yangu nikastuka risasi ikipiga kwenye kioo cha nyuma na kunifanya nirudi chini, na kulala kwenye siti yangu.Dereva akaanza kulalamika, na phidaya akaanza kumuhimiza dereva kuongeza mwendo kasi wa gari,risasi zipatazo nne zikaingia kwenye kioo cha nyuma cha gari na kushangaa ragi ikiaanza kuyumba huku dereva akiwa ameulalia mskani wake,

“shit dereva amepigwa risasi ya kichwa”
Phidaya alizungumza kwa kuchanganyikiwa kiasi kwamba na mimi nikaanza kuchanganyikiwa, risasi zikaendelea kumiminika ndani ya gari na kuzidi kunichanganya
“mtoe huyo dereva”

Nilizungumza kwa sauti ya juu, phdiaya akafanya kama nilivyo muagiza, akaufungua mlango wa dereva na kumsukumia kwa nje, kisha akafunga mlango na kukaa kwenye siti ya dereva

“nipe bastola yako”
Phidaya akanirushia kwa nyuma bastola yake, nikauchukua mkanda wa siti wa siti ya nyuma na kuanza kuuvuta nikijaribu kuukata ila nikashindwa.Nikamtazama
“eddy unataka kufanyaje?”
“nataka kukata huu mkanda niufunge mguu wangu unavuta sana”

Phidaya akafungua kwenye kisanduku kilichopo pembeni ya siti ya dereva, na kuanza kutoa vituvitu, vilivyomo ndani ya kisanduku, akabahatika kupata mkasi na kunikabithi.Nikauchukua mkasi na kuukata mkanda wa siti na kuufunga mguu wangu ulio vunjika, maeneo ya mapajani, hadi nilipo hakikisha kwamba nimeunguza misuli kuvuta, nikajilaza vizuri kwenye siti na kutoa magazine ya bastola na kukuta ikiwa na risasi za kutosha.

RIWAYA: She is My Wife- Sehemu ya 15 & 16

MUANDISHI : EDDAZARIA G.MSULWA 

ILIPOISHIA
“Fanya fasta basi”
Samson akatoka nje huku akiishika shika pua yake iliyo jaa maumivu ya kupigwa ngumi na Rahab, Samson akaingiza baiskeli ya kwanza na kutoka nje akiwa ameishika baiskeli ya pili akitaka kuingia ndani, gafla breki za gari aina ya Defender yenye askari wa kikosi cha F.F.U wapatao sita wakashuka kwenye gari kwa haraka huku wakiwa na bunduki na kunza kumfwata Samson sehemu alipo simama

ENDELEA
“Unafanya nini hapo?”
Askari mmoja alizungumza kwa sauti ya ukali na kumfanya Samson kuanza kutetemeka mwili mzima
“Husikii au?” askari aliendelea kuzungumza kwa sauti ya ukali
 
“Ni..ninaingiza baiskeli zangu ndani”
“Wewe kama nani?”
“Mimi, ni mmiliki wa hapa, mchana nilikimbia kutokana na tukio la majambazi”
Mazungumzo, yote yanavyo endelea nje Rahab anayasikiliza kwa umakini wa hali ya juu, huku bastola yake ikiwa mkononi mwake
“Mkuu tukague ndani”
Ombi  la askari huyu mwenye alama ya ‘V’ kwenye bega moja, likamfanya Samson kubaki akiwa anaduwaa, ila akajikaza asiuonyeshe mstuko wake kwani hakujua kitatokea nini baada ya askari hao kuingia ndani ya duka lake na kumkuta Rahab
“Kuna vurugu, maeneo ya Sinza kwa Remy, OVER”
Ilisikika sauti kupitia redio ya upepo aliyo ishika mkuu wao na kusababisha, kuto kulijibu ombi la asakri wake
“Tunakuja Over”
 
Alijibu, huku akiiwatazama askari wake na wote kwa pamoja wakarudi kwa haraka kwenye gari lao na kuondoka kwa kasi kubwa.Sammso akashusha pumzi nyingi, kwa haraka akaanza kuingiza baiskeli zake zote
“Tuondoke, tayari nimesha maliza”
Samson alimuambi Rahab na wote wakatoka nje kwa umakini, huku wakichunguza kila eneo la nje.Samson akapanda kwenye baiskeli yake
“Panda twende”
Rahab akaitazama baiskeli ya Samson kwa umakini,
“Siwezi kukivunja kiti chake”
“Wewe panda twende kwani kikivunjika tutajua mbele ya safari, isije hawa jamaa wakarudi na kunikuta tupo pamoja hapa sijui itakuwaje”
“Mmmm!!”
 
Rahab akapanda kwenye baiskeli na taratibu Samson akaanza kubadilisha gia moja baada ya nyingine zilizopo kwenye baiskeli yake kutoka gia laini kuelekea gia ngumu, na jinsi anavyozidi kuendesha baiskeli ndivyo mwendo wa baiskeli yake inavyozidi kuongezeka.Ndani ya dakika kumi wakawa wamefika nyumbani kwa Samson, wakaingia ndani kisiri pasipo mtu yoyote kuwaona
 
Ukimya ukatawala kati yao, na hakuna mtu aliye msemesha mwenzake kwa wakati huu, alicho kifanya Rahab, akavua viatu vyake na kupanda kitandani na kumfanya Samson kuendela kusimama akimtazama Rahab jinsi alivo jilaza chali akitazama paa la chumba chake
 
“Panda ulale”
Rahab alizungumza huku akimtazama Samson usoni
“Ahaa, mimi nitalala hapa chini”
“Wewe vipi, kinacho kuogopesha wewe ni nini?”
“Siogopi”
“Sasa kinacho kubabaisha ni nini, hebu acha ufala panda kitandani kwako ulale, ila onyo lala usiniguse mwili wangu”
“Mmmmm”
“Guna, tu”
“Ndio maana ninakuambia kwamba nitalala hapa chini”
“Sijawai kuona dume zima likiwa linaogopa kulala na mwanamke kitanda kimoja”
 
Samson akamtazama Rahab kwa umakini kisha akapanda juu ya kitanda na kuchukua mito miwili na kutengeneza mpaka kati yao ambao hakuna mtu ambeye angeweza kumgusa mwengine, Samson taratibu akajikuta akiaanza kutawaliwa na hisia za mapenzi juu ya Rahab ambaye anaonekana kawa si mtu wa masihara hata kidogo.Samson akauingiza mkono wake mmoja chini ya mto, na taratibu akanza kuupeleka katika eneo alilo lala Rahab.Akafanikiwa kuufikisha mkono wake alipo lala Rahab, akamminya kwenye maeneo ya mbavu , ila Rahab akatulia kimya na kujifanya kama amelala, Samson akarudia tena kumminya Rahab eneo la mbavu na Rahab hakuonyesha mtikisiko wowote
 
“Kitu kimelinki”
Samson alizungumza kimoyo moyo, huku usoni mwake akiachia tabasamu pana lililojaa uchu mkali wa mapenzi, akajigeuza na kujilaza kiubavu, taratibu mkono wake mmoja ukaanza kupandisha hadi kwenye chuchu ya Rahab, hata kabla Samson hajaukandamiza mkono wake vizuri kwenye chuchu ya Rahab, gafla macho yake yakakutana yakitazamana na jicho la bastola, aliyoishika Rahab kwa umakini
                                                                                           **************
Vyomo vingi vya habari ndani na nje ya nchi ya Tanzania vimepambwa na taarifa juu ya kukamatwa kwa majambazi sugu walio walaza askari wengi macho kwa kazi moja ya kuwatafuta popote walipo, usiku na mchana.Sura za Fetty, Anna, Halima na Agnes zimepamba magazeti mengi ikiwemo hata magazeti ya udaku,askari walio fanikisha kukamatwa kwa majambazi hawa, ikawa ni moja ya ofa kubwa katika maisha yao kwa kila mmoja kupandishwa cheo kimoja kutoka sehemu alipo hadi sehemu ambayo mkuu wa majeshi Raisi wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania alihisi inastahili kwao.

Japo kuna misiba mingi ya askari walio kufa katika oparesheni kimbunga ya kuwavamia majambazi hao, familia za askari walio kufa zikapewa kiasi cha shilingi milioni mia moja, pamoja na bima za matibabu kwa wale askari wote walio na tattoo chini ya umri wa miaka kumi na nane
 
Ila haikuwa furaha kwa dokta Wiliam ambaye yupo nchini mwao kwa ajili ya likizo ya muda mrefu, jambo ambalo linazidi kumuumiza kichwa ni kuhusu mahali alipo jificha Rahab kwani hakuwepo katika orodha ya walio kamatwa, akaitoa simu yake ya mkononi na kuingiza namba za rais wa Tanzania, kabla hajapiga akaanza kujiuliza mswali yasiyo na majibu kichwani mwake
 
“Nikimpigia ninamuambia nini, je akiniuliza ilikuwaje nikawaagiza kwenye tukio hilo walilo lifanya itakuwaje?”
Dokta William alijiuliza swali ambalo akabaki akiitazama namba ya rais, taratibu akakishusha kidole gumba cha mkono wa kulia, ulio ishika simu yake na kuiminya batani yenye alama ya kijani, inayo ashiria kuwa ndio batani ya kupiga simu, akaiweka sikioni simu yake huku mwili ukimtetemeka kiasi kwamba akabaki akiwa anameza mafumba ya mate mengi, ndani ya sekunde kadhaa sauti nyororo kutoka upande wa pili wa simu ukaanza kusikika
“MTUMIAJI WA SIMU UNAYE MPIGIA, ANAONGEA NA SIMU NYINGINE. TAFADHALI SUBIRI AU KATA SIMU NA UPIGE TENA”
 
Dokta William akakata simu yake na kushusha pumzi nyingi huku akiitazama, akaiingiza simu yake mfukoni na kunyanyuka kwenye kochi lake alilo likalia, kabla hajafanya chochote akasikia simu yake akiita, kwa haraka akaitoa na kukuta namba ya rais ikiingia, akaipokea na kuiweka simu yake sikioni
 
"Ndio muheshimiwa raisi"
"Niliona simu yako ikiingia Dokta William"
"Ndio muheshimiwa, ila nilitaka tuzungumze kuhusiana na hao mabinti walio kamatwa napolisi"
 
"Una maoni gani juu yao?"
"Hao ndio wale vijana ulio niagiza kufanya nao kazi ya kuwasaka wote, wanao isumbua serikali yako"
"Kwa hiyo mimi nifanyeje?”

"Usiwachukulie sheria kali bado tunawahitaji"
"Siwezi kufanya ujinga kama huo kwasababu wametugharimu sana serikali yetu"
Raisi alizungumza kwa hasira kisha akakata simu, na kumuacha Dokta William akibaki akiitazama simu yake pasipo kuzungumza kitu cha aina yoyote
 
     ******
Mwili wa Samson ukaanza kutetemeka, baada ya macho yake kutazamana na bastola ya Rahab
“Nilikuambia usiniguse, mimi sio Malaya sawa?”
Rahab alizungumza kwa sauti ya ukali
“Sawa mama”
 
Samson ili kuepukana na dhahama ya kupigwa risasi na Rahab taratibu akajishusha chini, akachukua taulo lake na kulilaza sakafuni na kujilaza.Masaa yakazidi kutakika hadi asubuhi ambapo Samson akawa wa kwanza kustuka kutoka usingizini, hii ni kutokana na ubaridi mkali uliompiga kwenye sakafu, akatoka nje na moja kwa moja akakimbilia chooni kutoa haja ndogo iliyo mbana sana kisha akarudi chumbani kwake
 
Akamkuta Rahab akiwa, anajinyoosha nyoosha huku akipiga miayo, Samson akamsalimia Rahab ila hakujibu kitu cha aina yoyote zaidi ya kumtazama tu.
“Simu yako ina redio?” Rahab aliuliza
“Ndio”
 
“Inashika stesheni gani?”
“TBC FM, Redio One , Clouse”
“Weka TBC”
Samson hakuwa mbishi zaidi ya kuiwasha simu yake, sehemu ya redio, wakakuta miziki ikiwa imerindima kwenye kituo hicho
“Weka stesheni nyingine”
 
Samson akatii na kuweka stesheni nyingine, hakuna stesheni iliyokua na kitu cha maana na kumfanya Rahab kujipa matumaini wenzake wapo katika hali salama.Samson akamuomba Rahab amsubirie anakwenda kuchukua kifungua kinywa
“Unakwenda kununua nini?”
“Mihogo ya kukaanga”
“Powa, chukua na gazeti”
“Gazeti la kufungia hiyo miogooo au gazeti la kusoma?”
“Wewe unaona gazeti gani?”
“Powa nimekuelewa”
 
Samson alizungumza huku akitabasamu, akatoka ndani kwake a kwenda mtaa wa pili ambapo kuna biashara za mihogo ya kukaanga, kifungua kinywa ambacho Samson anakipenda na pia kinarahisisha matumizi ya pesa yake, hii ni kutokana na kipande kimoja cha muhogo kuwa ni shilingi hamsini ya kitanzania, Samson akanunua magazeti mawili yaliyo na picha za wasichana ambao moja kwa moja akawatambua ni wale walio kuwa wakizipiga risasi kama wendawazimu.

Kwa mwendo wa haraka huku mkono wake mmoja akiwa ameshika kifuko chenye mihogo ya elfu moja na mkono wake mwingine akiwa na magazeti akafika nyumbani na kuingia ndani
 
“Oya kuna habari hapa sio nzuri”
Samson alizungumza huku akimpa gazeti, Rahab
“Habari gani?”
Rahab akachukua gazeti la Mwananchi na kuligeuza kurasa ya kwanza na kuwaona wezake wakiwa wapo chini ya ulinzi wa polisi, jasho jembamba lililo endana na mapigo ya moyo ya kasi vikaanza kuchukua nafasi kwa wakati mmoja, hakuamini kama wezake wamekamatwa, akafungua kurasa ya ndani na kushuhudia picha za wenzake wakiwa wanapandishwa kwenye magari ya polisi
 
“Inabidi tufanye kitu chochote kuweza kuwaokoa wezangu”
Rahab alizungumza huku mwili mzima ukiwa unamtetemeka
“Ufanye na nani?”
“Na wewe”
“Mimi?”
“Ndio”
“Siwezi”
Kwa haraka Rahab akasimama na kuichomoa bastola yake na kuiweka kichwani mwa Samson, huku mwili mzima ukiendela kumtetemeka kwa hasira kali, iliyomfanya kuyang’ata meno yake kwa nguvu zake zote
 

SHE IS MY WIFE(NI MKE WANGU)……16

“Basi basi, nitafanya”
Samson alizungumza kwa sauti ya kukata roho na kumfanya Rahab kumuachia, na kukaa pembeni, ukimya ukaanza kutawala kati yao, huku Samson macho yake yote yakiwa kwa Rahab aliye kaa kitandani huku amejiinamia chini
“Unaweza kutumia silaha?”
“Hapana”
Rahab akaachia msunyo mkali huku akimtazama Samson
                                                                                              *******
Mipango ya kuwapeleka Fetty na wenzake katika mahakama kuu inayoshuhulika na maswala ya kigaidi ‘THE HUNG’, ikaanza kufanyika kwa ulinzi mkali wa vikosi vyote vya ulinzi vilivyopo nchini Tanzania, tangu kukamatawa kwao maisha yao yamekuwa ni yakufungwa vitambaa vyeusi katika macho yao pamoja na kufungwa pingu ambazo ni toleo jipya na mara nyingi hutumika katika mataifa makubwa kama Marekani na Uingereza katika swala zima la kuwafunga wahalifu walio shindikana na serikali zao, wanao hesabiwa kama magaidi.
 
Waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali duniani wameweka kambi nje ya makao makuu ya jeshi la polisi, kila mmoja akisubiri kunasa habari ya ni siku gani magaidi hao wa kike watasafirishwa kupelekwa mahakamani, kwani kila mmoja anahamu sana ya kuwaona wasichana hao wanafananiaje kwani matukio waliyo yafanya tangu nchi ya Tanzania ipate uhuru mwaka 1961, hapakutokea kundi au watu walio iumiza serikali kwa kiasi kikubwa sana katika kuua idadi kubwa ya polisi kama walivyo fanya  Fetty na wenzake
 
IGP bwana G.Nyangoi kwa mara ya kwanza anajitokeza mbela ya waandishi wa habari huku akiwa ametawaliwa na tabasamu kubwa, kwani kuwakamata magaidi hawa kwake ni jambo kubwa la kufurahisha na ni miongoni mwa ushindi mkubwa tangu akabidhiwe kiti cha kuliongoza jeshi la polisi
“Nitakaribisha, maswali yasiyo zidi matano tu, ili kuokoa muda”
 
Bwana G.Nyangoi alizungumza mbele ya waandishi wa habara walio zitega kamera zao za aina mbali mbali 
 
“Mimi ni Jonh kutoka shirika la utangazaji la BBC Swahili, Ningependa kufahamu kama jeshi la polisi ni hatua gani ambazo mmepanga kuzichukua kwa askari wote walio kufa katika harakati za kuwakamata hawa magaidi?”
 
“Nilisha zungumza hapo awali, kwa wale askari wangu wote walio fariki katika tukio zima la kuwatafuta hawa magaidi, familia zao zimelipwa kiwango cha shilingi milioni mia moja, huku wale wenye watoto wao watasomeshwa na serikali kuanzia elimu ya msingi hadi chuo kikuu”
 
“Je, magaidi hao mmepanga kuwasafirisha kwa usafiri gani?”
“Magaidi, watasafirishwa kwa kutumia ndege”
“Ndege gani?”
“Ndege za jeshi zitahusika katika kuwapeleka mahakama kuu ya magaidi”
 
“Je, kwa nini wasihukumiwe hapa hapa nchini Tanzania hamuoni, kuwapeleka huko inagharimu kiasi kikubwa cha pesa?”
 
“Kwakiwango walicho kifikia hawa mabinti  ni kikubwa sana na kimefikia kiwango cha kuhesabiwa kama magaidi wa kimataifa na sisi kama washiriki wa umoja wa mataifa tunawaachia umoja wa mataifa kufanya kazi juu ya hawa watu, Asanteni sana kwa maswali yenu”
 
“Muheshimiwa swali moja la mwisho”
“Ehee uliza, ila hili ndio litakuwa swali langu la mwisho, ninawahi kikao sawa jamani”
 
“Tumesikia kwamba mmeshirikiana na FBI katika kuwakamata hawa mabinti , nyinyi mlishindwa kufanya hiyo kazi?”
 
“Hapana, vijana wetu wenye mafunzo kamili ndio wameifanya hiyo kazi, Asanteni sana”
IGP Bwana G.Nyangoi akawaaga waandishi wa habari na kuingia zake ndani na kuwaacha wakiwa wanaulizana maswali wao kwa wao
                                                                                                ********
“Shiti…, huu ni ujinga”
Rahab alizungumza huku akiitazama Tv ndogo iliyomo kwenye chumba cha Samson, kwa kupitia chaneli ya Star Tv aliweza kuyaona mahojiano  ya waandishi wa habari na mkuu wa jeshi la polisi bwana G.Nyangoi
 
“Tutafanyaje, wakati watu ndio hao tayari wamekamatwa?”
Samson aliizungumza huku akimtazama Rahab aliye ikunja sura yake, Rahab akainyanyua sura yake na kumtazama Samson kisha akairudisha kwenye Tv inayoonyesha miziki ya bongo Flevar
“Tunaweza kuwapata”
“Tutawapataje?”
“Nitakuonyesha jinsi ya kuwapata”
                                                                                                

************
Rahab anafanikiwa kufika katika uwanja wa ndege wa Julias Kambarae Nyerere, bila ya mtu yoyote kuweza kumgundua, kwa jinsi alivyo jitanda mtandio kichwani na kujipara vilivyo, haikuwa rahisi kwa mtu yoyote kuhisi kama yeye ni jambazi, kitu cha kwanza kukifanya anamtafuta Ludovirk mwanaume ambaye alishawahi kulala naye kipindi cha nyuma akiwa anafanya kazi ya kujiuza mwili wake, na Ludorvick anahusika katika kitengo cha ukaguzi.

Kwa bahati nzuri akamuona Ludorvick akiwa amesimama kwenye moja ya nguzo, huku akizungumza na simu.Kwa mwendo wa umakini Rahab akatembea hadi sehemu alipo simama Ludorvick na kumgusa bega kwa nyuma
“Ludo”
Rahab aliita kwa sauti ya uchokozi ambayo ni nyepesi sana, na iliyo legea.Ludovick akageuka na kukutana na Rahab
“Sawa ngoja nitakupigia kuna kazi ninaifanya mara moja hapa”
 
Ludorvick alimjibu mtu anaye zungunza naye kwenye simu, akaikata simu yake na kumkumbatia Rahab kwa nguvu
“Upo wewe?” Ludorvick alizungumza kwa sauti ya mshangao, na iliyo jaa furaha sana
“Ndio nipo”
“Umezidi kupendeza, mpenzi wangu”
“Asante”
 
“Twende ofisini, hapa si unaona jinsi watu walivyo wengi”
Ludorvick akaongozana na Rahab hadi ofisini kwake, huku njiani Rahab akiwatazama askari kwa umakini na hakuna ambaye anamfwatilia, wakaingia ofisini mwa Ludorvick, kitu cha kwanza alicho kifanya Ludorvick ni kuanza kuing’ang’ania midomo ya Rahab na kuanza kuinyonya kwa fujo, huku akiachia pumzi nyingi.Rahab hakutaka kujibana na akamuacha Ludorvick kufanya yake
“Mmmm, baby tupo ofisini banaa”
Rahab alizungumza kwa sauti ya kudeka
“Ngoja kwanzaa, kidogo”
 
Ludorvick alizungumza huku akiaanza kuvua koti lake la suti
“Jamani baby ngoja kwanza tuzungumze, leo nitalala na wewe usiku kucha”
“Kweli” Ludorvick alizungumza huku akihema kama bata mzinga
“Ndio baby, usijali kwa hilo”
 
Rahab alizungumza kwa sauti ya kudeka na kuzidi kumpagawisha Ludorvick, mchaga huyu anaye babaika sana kwenye swala zima la mapenzi, na kila anapovuta hisia siku aliyo pewa penzi motomoto na Rahab basi anajikuta mwili mzima ukimsisimka.

Ludorvick akaliokota koti lake la suti, alilokuwa amelitupa chini, Rahab akakaa kwenye kiti kilichopo karibu na meza ya Ludorvick
“Niambie mke wangu”
“Safi, tuu.Mume ninishida”
“Unashida gani mke wangu, mtoto mzuri kama wewe?”
“Mmmm, kuna shida nahitaji unisaidie”
“Zungumza, kama ni pesa wewe niambie tu nitakupa kiasi chocote utakacho kihitaji”
 
Kabla Rahab hajazungumza kitu simu ya mezani mwa Ludorvick ikaita na kumfanya Ludorvick kuachia msonyo mkali na kuipoke na kuminya kitufe cha kuifanya sauti kuwa kubwa(Luodspeker)
 
“Ludorvick andaa ndege yangu, ninasafari saa mbili na nusu usiku, hakikisha inakaguliwa vya kutosha”
Sauti nzito ilizungumza kutoka upande wa pili wa simu
“Sawa sawa, mheshimiwa Raisi”
Simu ikakatwa na Ludorvick akabaki akiwa ameduwaa kwani hakutegemea kupokea simu ya Raisi kwa wakati kama huu,
“Nani?’
“Raisi”
“Mmmmm”
“Yaani hapa amesha nivunja nguvu mke wangu?”
“Kwa nini?’
“Ndio nilikuwa ninataka kutoka kazini, hapa itanibidi nikasimamie zoezi zima la ndege yake kukaguliwa , hadi aondoke nchini na sijui anakwenda wapi”

“Twende nikakusaidie mpenzi wangu, uku unafanya kazi ninakupeti peti”
“Eti eheee”
 
“Ehee, kwani sipaswi kuwa karibu nawe?”
“Unapaswa, ngoja niwapigie simu wakaguzi wangu”
Ludorvick akawapigia simu wakaguzi wake wanaohusika katika ukaguzi wa ndege na kuwapa kazi hiyo na kuwaamuru waanze mara moja pasipo kupoteza muda.

Ludorvick akatoka na Rahab hadi sehemu ya maegesho ya ndege ya Rais na kuwakuta watu wake  akiwa katika kazi ya ukaguzi wa ndege ya Rais  Praygod Makuya, ambayo ni aina ya ‘Air Force’ aliyopewa na serikali ya Marekani, katika kuimarisha ulinzi katika safari zote za raisi wa Tanzania
 
“Kumbe Raisi anandege kubwa kama hii?”
“Ndio, hii Raisi alipewa kama msaada, si unajua Marekani na TANZANIA tunashirikiana katika mambo mengi”
“Ahaaaa, kwa hiyo humo ndani anaingia Raisi peke yake au?”
“Humo anaingia Raisi na wajumbe wake wote”
“Ahaaa”
 
“Twende ukaone ndani”
Ludorvick alizungumza huku akiongozana na Rahab kupandisha ngazi ndefu kuelekea juu ulipo mlango wa kuingilia ndani kwenye ndege kubwa, ambayo ukiachilia ukubwa na ubora wa ndege anayo tembelea Raisi wa marekani, inayo fwata ni ndege hii anayo tembelea Raisi wa Tanzania Dokta Praygod Makuya.

Macho ya Rahab yakawa na kazi ya kutazama sehemu zote za ndani ya ndege
“Hii ndege, wamarekanai wameweza kutengeneza, kwa maana inavitu vingi sana vya kumlinda Raisi”
“Ahaaaa, natamani niipande na mimi kuwa miongoni mwa abiria”
 
“Ahaaa hii huwezi kupanda, ukiachilia ikulu ya raisi, akiwa hewani Raisi Ikulu yake inakuwa humu ndani na ndani ya hiyo ofisi anaweza kufanya kazi zake zote kama akiwa ardhini”
 
Ludorvick akaendelea kumuelekeza sehemu mbali mbali za kwenye ndege hii ya kisasa ya Raisi wa Jamuhuri wa muungano wa Tanzania bwana Praygod Makuya.Pasipo Ludorvick kuona,
“Baby ninakuomba niingie chooni”
“Sawa ngoja mimi niingie kwenye chumba cha marubani niaangalie kama kuna usalama”
“Sawa”
 
Rahab akachukua nguo nne za wahudumu wa ndege ya Raisi na kuingia nazo chooni pasipo Ludorvick kuona tukio hilo, akazikunja vizuri na kuzificha kwenye makalio yake kisha alipo hakikisha kwamba yupo vizuri akatoka chooni na kumkuta Ludorvick akimsubiria
“Umeona hivyo vyoo vilivyo vizuri”
“Ndio, hivi wahudumu wa Raisi wanaingia saa ngapi ndani ya ndege?”
“Lisaa limoja kabla ya raisi kuingia ndani ya ndege”
Ludorvick na Rahab wakatoka kwenye ndege na kwenda sehemu ya kutokea, nje ya uwanja wa ndege kwa kupitia geti la nyuma ya uwanja
“Baby ngoja nikupe pesa, uchukue taksi mimi ngoja nirudi nikawasimamie hawa vijana”
“Sawa”
 
Ludorvick akatoa laki mbili na kumkabithi Rahab
“Alafu sijachukua namba yako ya simu”
“Sina simu mume wangu”
“Ohooo basi ngoja nikuongezee pesa ukanunue nyingine”
“Sawa nitashukuru”
Ludorvick akatoa laki na nusu na kumkabithi Rahab kisha akamtajia namba yake ya simu na Rahab akaahidi kuishika kichwani mwake
“Sawa baby nitakupigia”
Rahab akaondoka huku akiwa na furaha kubwa moyoni mwake, akachukua taksi hadi nyumbani kwa Samson na kumkuta Samson akiwa amejilaza kitandani huku akionekana kuwa na mawazo mengi
“Umetoka wapi?”
Samson alizungumza kwa sauti ya ukali, huku akimtumbulia mimacho Rahab
 
“Unaniuliza wewe kama nani?”
“Sio ninakuuliza kama nani, ila nataka kujua unatatoka wapi kumbuka kwamba hapa upo kwangu?”
“Hupaswi kujua, mwehu nini wewe?”
Samson akanyanyuka kwa hasira na kumzaba Rahab kibao cha shavuni kilicho myumbisha hadi kikamuangusha chini
 
ITAENDELEA...
© Copyright MZALENDO HURU
Back To Top