Featured
Loading...

RIWAYA: Sorry Madam - Sehemu ya 59 & 60 (Riwaya inawafaa kuanzia miaka 18 na kuendelea )


 Mtunzi : Eddazaria g.Msulwa


Ilioishia...
Hadi kunapambazuka sikuweza kumuona nesi phidaya, hali ya hatari ikaanza kunijia kichwani mwangu na kuhisi nesi phidaya anaweza kuwa amekutwa na matatizo, mlango ukafunguliwa na wakaingia manesi wawili pamoja na madaktari wale wawili.Wakaanza kufungua kitandana na kukishusha chini kidogo hadi kikafikia usawa mzuri wa kuweza kusukumwa.Pasipo hata ya kunisemesha wakaanza kunisukuma na kunipeleka nisipo pajua huku nyuso zao zikiwa na tabasamu ambalo sikuliewewa nini maana yeke

Endelea...
Wakazidi kukisukuma kitanda nilicho lalia hadi hadi tukafika kwenye maja ya mlango ambao juu kuna maandishi ya kiharabu ambayo sikuweza kuyaelewa, nesi mmoja akausukuma mlango na kufunguka, na wakaniingiza ndani nikiwa juu ya kitanda changu, mwanga mwekundu wa taa ulioo ndani ya chumba ukazidi kuniogoesha.Chumba kizime kimezungukwa na mashine mbalimbali ambazo sikujua zinakazi gani.Daktari mmoja akachukua mashine yenye kimviringo mbele, kisha akakiwasha na kuanza kuzunguka, akachukua moja ya miwani kubwa ambayo ni nyeupe akaivaa na kuanza kucheka kitu kilichoo zidi kuniogopesha zaidi.

Gafla taa ya mwanga mweue ikawashwa na kuwafanya madaktari na manesi, kustuka, macho yetu wote tukayaelekezea mlangoni na kumuona nesi phidaya akiwa ameshika, bastola huku jasho jingi likiwa linamwagika usoni, akaanza kuzungumza kwa kiarabu na taratibu madaktari wakanyoosha mikono juu wakitetemeka, akazungumza neno lililo wafanya  madaktari kuanza kurudi nyuma kutoka kilio kitanda changu.
“eddy, wamekufanya chochote kibaya?”
“hapana”
“powa”

Nesi phidaya akazungumza neno jengine lililowafanya madaktari na manesi kulala chini, sakafuni huku mikono yao wakiwa wameiweka juu ya vichwa vyao.Nesi phidaya akanifwata hadi kitandani na kuuitisha mkono wake mmoja kwenye, mgongo wangu na kuniomba niwe kushuka chini, japo ninajihisi maumivu ila nikajikaza kiume kwani kuendelea kukaa haoa kutahatarisha maisha yangu.
“jikaze baba yangu”

Nesi phidaya alizungumza huku akiendelea kunishusha kwenye kitanda, akanisaidia kusimama vizuri, huku muhimili wangu wote wa kusimama nikiutegemea kutoka kwake, nesi phidaya akawatazama watu madaktari walio lala chini, akazungumza neno la ukali lililo wafanya madaktari na manesi kuzidi kuzifunika sura zao chini pasipo kuzinyanyua juu.Tukafanikiwa kotoka nje ya chumba walicho niingiza, nesi phidaya akafunga mlango kwa nje na sote tukaanza kuondoka taratibu huku nesi phidaya akiificha bastola yake na baadhi ya wahudumu wakabaki wakiwa wanatushangaa.Tukatoka nje na kukuta gari aina ya taksi ikiwa inatusubiria

“ahaaaa”
Nilitoa mguno wa maumivu baada ya mguu wangu nilio vunjika kugongwa kwenye mlango nilipokuwa ninajiaandaa kuingia ndani ya gari, siti ya nyuma
“pole eddy”
“asante”

Nesi phidaya akanisaidia kuingia ndani ya gari na kufunga, kisha yeye akaingia kwenye siti ya mbele kwa dereva na kumuongelesha dereva kiarabu na akaliondoa gari lake kwa kasi.
“asante sana, nesi phidaya”
“usijali nipo kwa ajili yako, ila ningependa uniite phidaya tu na si nesi phidaya”
“sawa”

Nikaendelea kujilaza kwenye siti ya nyuma ya taksi tuiyo ipanda, ila kuna mwanga mkali wa taa ukawa unaingia kwenye gari letu, ikanilazima kunyanyua kichwa changu kutazama nyuma, nikaona gari ndogo ikija kwa kasi sana,
“phidaya kuna watu wanatufwata nyu……”

Kabla sijamalizia sentesi yangu nikastuka risasi ikipiga kwenye kioo cha nyuma na kunifanya nirudi chini, na kulala kwenye siti yangu.Dereva akaanza kulalamika, na phidaya akaanza kumuhimiza dereva kuongeza mwendo kasi wa gari,risasi zipatazo nne zikaingia kwenye kioo cha nyuma cha gari na kushangaa ragi ikiaanza kuyumba huku dereva akiwa ameulalia mskani wake,

“shit dereva amepigwa risasi ya kichwa”
Phidaya alizungumza kwa kuchanganyikiwa kiasi kwamba na mimi nikaanza kuchanganyikiwa, risasi zikaendelea kumiminika ndani ya gari na kuzidi kunichanganya
“mtoe huyo dereva”

Nilizungumza kwa sauti ya juu, phdiaya akafanya kama nilivyo muagiza, akaufungua mlango wa dereva na kumsukumia kwa nje, kisha akafunga mlango na kukaa kwenye siti ya dereva

“nipe bastola yako”
Phidaya akanirushia kwa nyuma bastola yake, nikauchukua mkanda wa siti wa siti ya nyuma na kuanza kuuvuta nikijaribu kuukata ila nikashindwa.Nikamtazama
“eddy unataka kufanyaje?”
“nataka kukata huu mkanda niufunge mguu wangu unavuta sana”

Phidaya akafungua kwenye kisanduku kilichopo pembeni ya siti ya dereva, na kuanza kutoa vituvitu, vilivyomo ndani ya kisanduku, akabahatika kupata mkasi na kunikabithi.Nikauchukua mkasi na kuukata mkanda wa siti na kuufunga mguu wangu ulio vunjika, maeneo ya mapajani, hadi nilipo hakikisha kwamba nimeunguza misuli kuvuta, nikajilaza vizuri kwenye siti na kutoa magazine ya bastola na kukuta ikiwa na risasi za kutosha.

Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )
© Copyright MZALENDO HURU
Back To Top