AFYA ya aliyekuwa staa wa timu ya taifa ya Brazil,
Pele inazidi kuimarika baada ya kufanyiwa upasuaji wa tezi dume katika
Hospitali ya Albert Einstein mjini Sao Paulo nchini Brazil.
Hospitali hiyo imeeleza kuwa Pele mwenye umri wa miaka 74 anaendelea vizuri baada ya upasuaji huo uliofanyika wiki hii.
Pele aliwahi kulazwa katika hospitali
hiyo takriban miezi sita iliyopita kwa upasuaji wa dharura ili kuondoa
mawe katika figo yake.
Pele ambaye jina lake ni Edson Arantes
do Nascimento alifunga zaidi ya mabao 1200 wakati alipokuwa akicheza
soka na kuisaidia Brazil kushinda mataji matatu ya kombe la dunia.
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )