Mwanafunzi
 wa kidato cha sita wa Shule ya Sekondari Thaqaafa ya jijini hapa, Amos 
Kitala (26) ameuawa kwa kuchinjwa kwa kipande cha chupa shingoni kwenye 
kilabu cha pombe za kienyeji.
Kamanda
 wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Justus Kamugisha alisema tukio hilo lilitokea
 Machi 19, mwaka huu saa 10 jioni wakati mwanafunzi huyo akigombana na 
watu wawili kwenye kilabu hicho.
Kamugisha
 alisema inadaiwa kabla ya kuuawa Kitala alionekana kuwazidi nguvu 
wagomvi wake na ndipo walipoamua kuchukua chupa, kuivunja na kumkata 
nayo shingoni na kusababisha atokwe damu nyingi.
Kamgisha alisema wanamshikilia Ramadhan Sima (27) na Omary Philipo (35) kwa tuhuma za mauaji hayo.
Wakati
 huohuo; kibarua amekufa kwa kudondoka kutoka kwenye lori alilokuwa 
akining’inia wakati akidai ujira wa Sh10,000 kwa kupakia kokoto.
Kamugisha
 alimtaja kibarua aliyepoteza maisha baada ya kudondoka kwa kile 
kilichodaiwa ni kusukumwa na dereva wa lori hilo aina ya Scania kuwa ni 
Mashaka Mathias (34), mkazi wa Isamilo.
Dereva huyo, Haji Juma (38) anashikiliwa na polisi kwa mahojiano kuhusiana na kifo cha kibarua huyo.
Katika
 tukio jingine; Christopher Starabu (34), amefariki dunia baada ya 
kugongwa na gari wakati akivuka barabara katika eneo la Mabatini.
Kwa mujibu wa Kamugisha, dereva wa gari hilo, Rajabu Mika (30, Mkazi wa Bwiru anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za mauaji hayo.
Mwalimu wa Shule ya Msingi Ilula, John Sinega (29), amefariki dunia baada ya kugongwa gari wakati akiendesha pikipiki.
Kamanda
 huyo alisema, dereva wa gari hilo, Ismail Jamal (36), anashikiliwa na 
polisi kwa tuhuma za kusababisha kifo cha mwalimu huyo.
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )
