Inadaiwa nyumba hiyo ilinunuliwa na
Gekul kwenye mnada ulioendeshwa na benki ya makabwela ya NMB mwanzoni
mwa mwezi uliopita kisha akampangishia mtu aliyeondolewa juzi na
madalali wa benki ya CRDB.
Akizungumza jana kwa njia ya simu, Gekul
alisema yeye aliinunua nyumba hiyo kupitia mnada uliondeshwa na NMB
kumbe huyo mtu aliyekuwa anaimiliki alichukua mkopo kwenye benki mbili
pamoja na CRDB ila haki yake haitapotea.
“Mimi nimewekeza mjini Babati nikiwa
mzalendo nikiona siyo lazima niwekeze jijini Dar es salaam, Arusha au
Dodoma, kwani napenda kuishi na wananchi wangu ila huyo mpangaji wangu
hata taarifa hakupewa,” alisema Gekul.
Alisema tangu ainunua nyumba hiyo
imepita mwezi mmoja ila mwanasheria wake anafanyia kazi suala hilo
kuhakikisha kuwa anapata haki yake hivyo wakazi wa mji wa Babati wasiwe
na wasiwasi wowote juu ya tukio hilo.
Hata hivyo, baadhi ya wakazi wa mji huo
walidai kuwa suala hilo linaendeshwa kisiasa kwani Gekul alinunua
kihalali nyumba hiyo ilipo karibu na shirika la Sido ambayo iliuzwa kwa
mnada hadharani baada ya benki ya NMB kuiuza.
“Mji wa Babati hivi sasa upo chini ya
Chadema kwani mbunge Gekul ni Chadema na pia halmashauri ya mji wa
Babati ni Chadema, hivyo wapinzani wetu wanatumia nafasi hiyo
kutuhujumu,” alisema John Tluway mkazi wa mji huo.
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )