Siku tatu baada ya kuibuka kwa kashfa ya rushwa miongoni mwa wajumbe wa Kamati za Kudumu za Bunge, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) imemuita Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe kumhoji.
Muda
 mfupi baada ya taarifa za kashfa hiyo kuwa wazi, Zitto na mwenzake wa 
Nzega Mjini, Hussein Bashe ambao ni wajumbe wa Kamati ya Huduma za 
Jamii, walimuandikia barua Spika wa Bunge, Job Ndugai kujiondoa kwenye 
nafasi zao ili kupisha uchunguzi dhidi ya tuhuma hizo.
Zitto
 alithibitisha kupata wito kutoka makao makuu ya Takukuru ili kuhojiwa 
juu ya sakata hilo na akapongeza kuwa endapo vyombo vya Serikali 
vitakuwa makini kushughulikia tuhuma zote zinazoelekezwa kwa wanasiasa 
na watumishi wengine wa umma, itasaidia kuongeza uwajibikaji na 
kupunguza uzushi kwa wananchi.
“Nimepata
 wito huo kupitia Ofisi ya Bunge. Nasikia Bashe ameitwa pia. Nafurahi 
wito wetu wa uchunguzi umechukuliwa kwa uzito unaostahili na tutatoa 
ushirikiano wote kwa vyombo vya uchunguzi ili kumaliza zoezi hili kwa 
haraka na kwa ufanisi,” alisema Zitto.
Alipotafutwa Bashe ili kupata ukweli wa kuitwa kwake, ingawa hakutimiza ahadi yake, alisema:“Sipo kwenye nafasi nzuri ya kuzungumza hivi sasa.”
Mpaka
 jana, wakati Takukuru ikiendelea kuwahoji wanasiasa na watendaji wa 
mashirika yaliyotajwa kuhusika kutoa rushwa ili kubadili maoni ya 
wajumbe juu ya utendaji wao, wabunge wawili walithibitika kuitwa na 
Takukuru.
Tuhuma
 hizo zimekwenda sambamba na Ndugai kuwaondoa wenyeviti wa kamati za 
Ardhi, Maliasili na Utalii; Nishati Madini; Uwekezaji na Mitaji ya Umma 
huku ile ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) na Huduma na Maendeleo ya
 Jamii lakini akisema ni uhamisho wa kawaida
 Mkurugenzi
 Mkuu wa Taakukuru, Valentino Mlowola, bila  kuingilia uchunguzi 
unaoendelea alithibitisha kuwaita wabunge hao na watendaji wa mashirika 
 waliohojiwa.
“Hili
 ni suala la uchunguzi Bado linaendelea hivyo si wakati muafaka kutaja 
watu waliohojiwa mpaka sasa ingawa mahojiano yanaendelea. Kazi 
ikikamilika utapata taarifa kamili,” alissema Mlowola.
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )
