Mei 6 2016 ilikuwa ni zamu ya Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Charles Mwijage kuwasilisha Bungeni Dodoma Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2016/2017.
Baada ya uwasilishaji huo Wabunge walipata nafasi ya kuchangia maoni yao kuhusu bajeti hiyo, hapa nakukutanisha na Mbunge wa Muleba Kusini Profesa Anna Tibaijuka alivyosimama na kutoa mchango wake..
>>’Mimi
ninafahamu kama Mwanauchumi ni lazima viwanda vinaendana na kilimo,
huwezi kuendeleza viwanda kama hujaendeleza kilimo. Ni lazima tuwe na
malighafi kwamfano mazao ya mchele na alizeti‘
‘Mimi
kama mchumi ntasema kwamba Taifa hili halina sababu yoyote isipokuwa
katika hali ya dharura kukubali kuagiza sukari, mchele au alizeti kutoka
nje, lazima kuwe na mkakati wa kulinda viwanda‘
‘Hali hiyo tujipange
sasa, tulio wengi ni wakulima, wavuvi na wafugaji. Sasa mnatuwezeshaje?
ninaposema sukari isiingie, ikiingia itaua viwanda vya sukari.. hata
mtoto wa shule anajua hilo, lazima Wizara iwe na utaratibu wa kuingiza
sukari lakini sio kutumia wafanyabiasharaTupe Maoni Yako( Matusi Hapana )