Kila siku
asubuhi huwa nazisogeza headlines zilizobebwa kwenye kurasa za Magazeti
ya Tanzania, Uchambuzi wa stori zote napandisha kwenye account yangu ya
Twitter >>>@millardayo. Tayari nimezikusanya na waweza
kuzipitia hapa chini moja baada ya nyingine.
Moja ya stori iliyoripotiwa ni hii kwenye gazeti la Habari Leo yenye kichwa cha habari ‘Mwarobaini wizi wa bodaboda wapatikana’
Gazeti
hilo limeripoti kuwa mamlaka ya elimu na mafunzo ya ufundi stadi ‘VETA’
imebuni kifaa cha kudhibiti wizi wa magari na pikipiki za abiria maarufu
bodaboda kwa kutumia simu ambapo kwa
kutumia kifaa hicho, dereva atakuwa na uwezo wa kuzima pikipiki au gari
kwa kutumia simu ya mkononi ambayo namba yake itakuwa imefungwa katika
chombo hicho.
Akizungumzia
kuhusu kifaa hicho Mwalimu wa Teknolojia ya mwasilliano wa VETA ,
Valerian Sanga alisema alishirikiana na mwalimu mwenzake wa chuo hicho
anayefundisha masuala ya umeme, Christian Brighton kubuni kifaa hicho
kilichowachukua miaka miwili.
Sanga
alisema kifaa hicho kina GPS na kinatumia mawasiliano ya simu kwa
kutumia GSM itakayosaidia kujua sehemu pikipiki au gari lilipo, lakini
pia kikimwezesha mmiliki kuzima na kuwasha usafiri wake popote ulipo
pia sasa wanafunga kifaa hicho kwa gharama ya sh 400,000 lakini wanatarajia baadaye watakapopata oda nyingi, watapunguza bei.
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )