July 31 2016 m
wili wa marehemu Mwanahabari Joseph Senga umeagwa
Dar es salaam leo kuelekea Mwanza kwa ajili ya maziko, baadhi ya
viongozi wa serikali na siasa wameshiriki wakiwemo Waziri wa habari,
utamaduni, sanaa na michezo Nape Nnauye, Waziri mkuu wa zamani Edward Lowassa na wengine.
Marehemu
Joseph Senga ndiye mpiga picha aliyenasa tukio la mauaji ya Mwandishi wa habari wa kituo cha talevisheni
CHANEL 10 Daud Mwangosi kilichotokea
September 2 2012 katika
kijiji cha Nyololo,
Wilaya ya Mufindi mkoani
Iringa ambaye alifariki July 28 2016 akiwa India kwa matibabu ya ugonjwa wa moyo.
Ninazo picha kadhaa kutokea Sinza Dar es salaam ambapo ndipo kazi yote ilifanyika
Waziri wa habari, utamaduni, sanaa na michezo Nape Nnauye
Kutoka kushoto Edward lowassa, Nape Nnauye na Freeman Mbowe
Mke wa marehemu Joseph Senga (aliyevaa ushungi)
Wapigapicha na wanachama wa Press Photographer wakishiriki kubeba jeneza la marehemu
Hii hapa chini ni moja ya picha yake enzi za uhai
ULIIKOSA HII YA ONYO LA RAIS MAGUFULI KWA WANAOANZISHA MAANDAMANO
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )