Featured
Loading...

Hili Ni Moja Ya Madaraja Tunayopaswa Kuyajenga, Si UKUTA..

Ndugu zangu,
Picha hizo zinajieleza zenyewe. Hakika inapendeza kuona Watanzania kwa desturi zetu ni watu wenye kujumuika pamoja bila kutanguliza tofauti za kisiasa. Ndio maana ya kusema, kuwa hili la maandamano ya UKUTA ni balaa tunalojitakia huku waandaaji wakijua fika hivyo.
Tukumbuke, kwa mwanadamu, siku zote, chuki hupandikizizwa, chuki humeea na chuki huzaa chuki. Kamwe, mavuno ya chuki hayajapata kuwa ya heri.
Ni jambo la hatari kwa nchi, pale kikundi kidogo cha watu kinapoachwa kifanye mzaha na hata ushabiki kwa jambo lenye kupelekea maafa kwa wengi. Lililo bora ni kwa watu hao kuonywa mapema kuacha kufanya mzaha na ushabiki huo.
Maggid,
Zanzibar.(P.T)

Tuma Maoni


Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )
© Copyright MZALENDO HURU
Back To Top