Jokate alitumia ukurasa wake wa Instagram kumwaga sifa hizo na kudai
kuwa akiwa amenuna akisikia sauti ya Alikiba anajikuta anafurahi kwani
anavutiwa sana na sauti hiyo.
“Alikiba ni King wa kutoa ngoma baada ya ngoma, King asiye kuwa na
mbwembwe, ni mzuri kuliko wote, ni mfalme wa sauti ya kumtoa nyoka
pangoni. Nikinuna najikuta nafurahi nikisikia sauti yake, hapa
nimesikiliza ‘Nisamehe’ nairudia tu, Nisamehe ni wimbo wa taifa unakuja
kwa kasi ya ajabu”.Aliandika Jokate
Alikiba na Baraka the Prince wanategemea kuachia wimbo ambao utaiwa
‘Nisamehe’ ni wimbo wa Baraka the Prince ameshirikisha Alikiba.
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )