Featured
Loading...

DUDU Baya a.k.a Mamba Aichana Chana Clouds Fm, Amwagia Sifa Rubby


Msanii mkongwe na asiyesahaulika katika tasnia ya muziki wa kizazi kipya dudu baya amekivua nguo kituo cha clouds fm kwa kuwaita ni wanafki wakubwa, wanyonyaji wa wasanii, na wenye kuharibia wasanii ndoto za mziki wao
Mamba alitolea mfano wasanii wanazungushwa mikoani kwenye tamasha la fiesta na kuambulia ujira mdogo, huku akisema pesa wanayopata kwenye hilo tamasha huishia hukohuko mikoani na hurudi dar wakiwa wamepayuka hawana kitu mfukoni

Dudu alisema hayo akipokuwa kwenye kipindi cha usiku cha FRIDAY NIGHT LIVE... FNL kinachorushwa na EATV

Alienda mbali zaidi kwa kumpongeza msanii mwenye kipaji anayekuja juu ruby kwa kusema ametoka kwenye minyororo ya wafu FM akawasihi na wasanii wengine wamuige ruby kwani ameonesha mfano

Akionekana mwenye afya km alivyokuwa zamani, amesema wafu fm hawajapiga nyimbo zangu kwa miaka sita sasa lakini sijatetereka naendelea na maisha yangu kama kawaida

Wakati akiendelea kuwatolea uvivu clouds fm mtangazaji wa kipindi hicho sam misago alitumia mbinu ya ziada kumtoa kwenye kile akichokuwa nacho moyoni
Hata hivyo alipongeza redio ambazo zipo chini ya IPP km East africa radio, radio one, capital fm na kusema hajawahi kuombwa pesa na mtangazaji au dj yeyote wa kituo hicho ili wimbo wake uchezwe hewan
Amevitaka vituo vingine kuiga vyombo vya ipp media

Kwa maneno ya dudu baya ni dhahiri wasanii wengi ni watumwa wa baadhi ya media house

Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )
© Copyright MZALENDO HURU
Back To Top