Featured
Loading...

RIWAYA: She is My Wife- Sehemu ya 9 & 10

 
Muandishi : Eddazaria g.Msulwa

Ilipoishia...
Dokta Williama aliendelea kuwasikiliza wakuu hawa wa polisi ambao vyeo vyao vinawatambulisha kama ma RPC kwenye mikoa yao.Lifti ikafunguka na wote wakatoka ndani ya lifti.Askari hao wakaendelea kwa mwendo wa kasi na kuingia kwenye ukumbi wa mikutano.Dokta William akajiweka sawa nguo zake na kuingia ndani ya ukumbi huu.Gafla macho yake yakatazamana na midomo ya bastola alizo elekezewa na wakuu wa polisi waliokaa kwenye viti vyao huku wakioneka kukasirishwa sana na uwepo wake

ENDELEA....
IGP bwana Gudluck Nyangoi akwaamuru wezake kuziweka silaha zao chini na wakati
“Karibu dokra Willian”
Bwana G.Nyangoi alizungumza huku akitabasamu na kumfanya dokta William kushusha pumzi nyingi,kidogo wasiwasi ukaanza kumpungua.

“Jamani huyu ni miongoni mwa wanajeshi wa umoja wa matiafa,yupo hapa nchini kwa ajili ya mafunzo wa madaktari wa jeshi letu juu ya jinsi gani wanaweza kumtengeneza sura bandia”

“Dokta,kwanza samahani kwa kukuvunjia ratiba zako kwa maana haikuwa katika ratiba zako leo kama nitakuitaji hapa”
“Bila samahani mkuu”
“Karibu ukae”

Dokta William akaka kwenye kiti alicho onyeshwa na bwana Nyangoi,akawaytizama makamanda wote waliopo ndani ya ofisi na hapakuwa na hata mmoja anaye mfahamu zaidi ya IGP Gudluck Nyangoi.

“Jamani kama munavyo jua,sisi kama jeshi la polisi tumekubwa na msiba mkubwa sana wakupoteza vijana wetu katika tukio la jana usiku,Pia ni aibu kubwa kwetu sisi kama jeshi la polisi kwa kushindwa kupambana na majambazi ambao,sijajua ni vipi tulishindwa kuwazuia na kusababisha maafa makubwa kama haya”

Ukimya ukatawala,huku akili ya Dokta William ikiwa inajaribu kupanga kitu cha kuzungumza kabla hajaulizwa kwani ametambua umuhimu wake wa yeye kuwa hapa ni kuwashauri viongozi waliopo humu ndani

“Jamani ninawasililiza,nasubiri maoni yenu.Nini tufanye ili kuwakamata hawa watu na ninavyo sikia wao ni wasichana sasa sijajua inakuwaje wasichana kama hawa wanatushinda kirahisi rahisi?”

“Mkuu mimi ninaona,kwanza tudhibiti mipaka yote ya nchi jirani kwa maana kumbukeni kulikuwa na tishio la kundi la Al-Shabab kuivamia mlimani city.Sasa isije ikwa ndio hao wameanza kutekeleza mipango yao”

“Asante bwana Shaban Mbago,mwengine?”
“Mkuu mimi kuna swala ambalo bado silipatii picha,haiwezekani mpango ule wa kumsafirisha yele binti katika njia ya ardhini ulibumburuka.Swali ni je,ni nani aliye toa siri ile?”

Mapigo ya moyo ya dokta William yakaanza kwenda kasi,ila hakutaka kuiruhusu hali hii kuendelea kuundama moyo wake,akawatazama wakuu wa polisi waliopo eneo hili na kuwaona wengi wapo kimya kila mmoja akikosa cha kuzungumza.Dokta William akanyoosha kidole na bwana G.Nyangoi akampa ruhusa ya kuzungumza
“Wakuu wangu mimi ninajambo moja ninaomba nizungumze”
“Zungumza tuu,kwani ushauri wako ni mkubwa sana”

“Kuna hali ambayo inaendelea ndani ya jeshi lenu,kwa kipindi kifupi nilicho kaa katika nchi hii na kushirikiana na jeshi lenu nikagundua kuna hali amayo sio nzuri na endapo mukiacha ikikua na kukomaa,Siku hadi siku jeshi lenu litazidi kuzalilisha na kuteketea mwisho wa siku ile imani ya kusema kuwa Tanzania ni nchi ya amani itafutika katika vichwa vya watu wengi”

“Viongozi kwa viongozi hamuaminiani,hilo ni la kwanza.Pili viongozi mumekuwa ni watu wakuunda vikundi vikundi vya watu ambao munawatumia kwa maslai yenu binafsi na si ya taifa.Kwa mfano kuna magaidi ambao jeshi la polisi mulikuwa munawatafuta kwa kipindi kirefu sana.

Kutokana na uaminifu finyu wa baadhi ya viongozi magaidi wale wakaendelea kudumu na kuishi kwa kipindi kirefu pasipo serikali kuzungumza kitu cha aina yoyote.Kila mulipo kuwa munajaribu kwenda kuwakama walikuwa wanawakwepa na kubaki mukijiuliza mutafanya nini?”

“Kabla ya hichi kikao kuendelea,jiulizeni je hakuna wasaliti watako vujisha siri juu ya watu muna watafuta? Na kama wapo je kuna haja gani ya hichi kikao kuendelea kuwepo hapa?”

Ukumbi mzima ukakaa kimya,sura za makamanda wote wapolisi zikawa zikimtazama Dokta William ambaye amezungumza maneno ambayo wengi wao hawakuwa wanayafikiria kuyazungumza

“Musikalie kuunda tume kuchunguza vitu ambavyo munajua majibu yake kabla ya kuzungumza.Nyinyi ni jeshi,munatakiwa kuwa kitu kimoja na si kuwa katika mgawanyiko ambao utawakost garama ambazo si za msingi.Jaribuni kuiga baadhi ya mbinu za kijeshi katika mataifa makubwa yaliyo endelea,mfano Marekani na kadhalika.Nitatolea mfano mdogo tuu wa wa wale wanejeshi walio tumwa kwenda kumuua Osama Bin Laden,Gaidi ambaye sisi kama Israel alituumiza pia vichwa jinsi ya kumpata”

“Ila kikosi cha wanajeshi wachache walio tumwa kuumuua Osama,kilikuwa ni cha siri kubwa hata makamu wa raisi wa Marekani hakuwa analifahamu hilo,zidi ya raisi Obama na wasadizi wake,Na tukio zima lilipokuwa linaendelea walikaa kwenye chumba maalumu pasipo na mtu yoyote kuwa na mawasiliano ya simu ya mkononi,hata raisi mwenyewe alizuiwa kuwa na simu.

Huo ni mfano mdogo ila hapa hapa ninashanga muheshimiwa unaendeleza kikao ila kuna huyo bwana hapo anachati na simu chini ya meza,Je kuna umuhimu gani wa hichi kikao?”
Bwana Noel Muro akastuka na kuuingiza simu yake mfukoni baada ya kunyooshewa kidole na Dokta William.
“Muro ninaomba uzime simu yako”

Bwana G.Nyangoi alizungumza huku akimtazama bwana Muro
“Mkuu cha mwisho kukizungumza ninawaomba,muunde kikosi maaalumu cha siri kitakacho wa pambana na hili swala.Asanteni”
Dokta William akakaa kwenye kiti na viongozi wote wakampigia makofi wakimpongeza kwa ushauri wake alio utoa.

“Dokta Willim asante sana kwa ushauri wako mzuri sana.Mimi ningekuomba usaidiane na mimi kuunda kikosi kitakacho weza kuwasaka hawa majambazi.Nipo radhi kuwaishawishi serikali kuongezea mshahara”
Laiti IGP bwana G.Nyangoi angegundua mtu anaye muomba juu ya huo mpango ndio muhusika nambari moja wala asinge zungumza hayo maneno

Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )
© Copyright MZALENDO HURU
Back To Top