VIJANA
 watano wamefikishwa mahakamani kwa tuhuma za kumdhalilisha Rais Dk. 
John Magufuli na Jeshi la Polisi kutokana na mauaji ya askari polisi 
wanne waliouawa na majambazi katika eneo la Mbande na Vikindu, Dar es 
Salaam hivi karibuni.
Washtakiwa
 hao walifikishwa jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es 
Salaam mbele ya mahakimu watano tofauti na kusomewa mashtaka na Wakili 
wa Serikali, Salum Mohammed.
Walisomewa
 mashtaka mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Emmilius Mchauru, Huruma Shahidi, 
Margareth Bankika, Dk. Yohana Yongolo na Respicius Mwijage.
Akisomewa
 mashtaka, mshtakiwa Dennis Mtegwa anadaiwa Agosti 24, mwaka huu eneo la
 Ubungo External kupitia mtandao wa WhatsApp, aliweka maoni katika group
 linaloitwa Dsm 11 4u Movement, akisema ‘JPM sijui anawaza nini 
kichwani… hata samahani hajui au nilikosea hajui’, ‘nchi imefika hapa 
kwa sababu ya mtu mmoja aliyeamua kujilipua ufahamu wake’, ‘sijaona 
tatizo kwa hilo, ila kwa huyu bwana misimamo ambaye amesema msinijaribu 
na ilhali kajaribiwa na ubwabwa wa jubilee kusema yote’.
‘Siasa
 si chuki wala upinzani si uadui, ajifunze kushindana kwa hoja sio 
mitutu ya bunduki na mazoezi yasiyo na kichwa wala miguu ya polisi’.
Mshtakiwa Suleiman Saidi anadaiwa Agosti 25, mwaka huu maeneo ya Kigogo, kwa kutumia mtandao wa Facebook, aliandika ‘Safi sana aisee, mi naona wangekufa kama 20 hivi halafu Simon Sirro tumuulize mazoezi wanafanyia wake zao au’.
Katika
 kesi nyingine, mshtakiwa Juma Mtatuu akiwa eneo la Ocean Road, Agosti 
24, mwaka huu anadaiwa kuwa alituma ujumbe katika Facebook akisema ‘Huyu
 hata akifa ataenda peponi, na kufanya mazoezi kote kule wamekufa 
Mbagala, mimi nitakuwa wa kwanza kuandamana  kule Kahama, tarehe moja 
naelekea Kahama kwa Ukuta, mimi nitakuwa namba moja kushika bendera ya 
Ukuta, kifo kipo tuu, usiogope kwani mawe na mapanga yameisha’
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )
