Jumamosi ya December 9 2017 ni siku ya
furaha kwa watanzania na wapenzi wa muziki wa dansi kwa ujumla, hiyo
inatokana na Rais wa awamu ya tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr
John Pombe Magufuli kutangaza msamaha kwa wafungwa wakiwemo msanii
Nguza Viking maarufu kama Babu Seya na Mwanae Papii Kocha.
Papii Kocha na baba yake Babu Seya
Rais Magufuli ametangaza msamaha kwa
Babu Seya na mwanae Papii Kocha akiwa mjini Dodoma katika maadhimisho ya
miaka 56 ya Uhuru wa Tanzania na muda mchache baada ya taarifa hizo
kutoka watu mbalimbali tumeona wakioneshwa kufurahishwa na uamuzi huo wa
Rais Maguli.
Mkuu wa idara ya habari na mawasiliano
wa club ya Simba Haji Manara ni moja kati ya watu waliooneshwa
kufurahishwa na maamuzi hayo na kaamua kuandika hivi kupitia ukurasa
wake wa instagram katika picha ya Papii Kocha akiwa kavaa jezi ya Simba.
“Nchi imezizima sababu yenu . Mungu
ametenda miujiza kupitia kwa Rais wetu..uliitangaza Simba hadi
gerezani..ntakuvalisha jezi mpya iliosainiwa na wachezaji wote…ila Wenger bado hajatwaa taji…. kama ulivyomuacha”>>> Haji Manara
Huo ni ujumbe wa Haji manara kupitia
ukurasa wake wa instagram, kama utakuwa unakumbuka vizuri Babu Seya na
watoto wake watatu akiwemo Papii Kocha walihukumiwa kifungo cha maisha
jela mwaka 2004 baada ya kukutwa na hatia ya kesi ya kubaka na kunajisi
watoto 10.
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )