Featured
Loading...

Takukuru kumfikisha mahakamani Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), Sadifa Juma Khamis

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) Mkoa wa Dodoma imesema Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), Sadifa Juma Khamis atafikishwa mahakamani leo.

Kamanda wa Takukuru mkoani Dodoma, Emma Kuhanga jana alisema Sadifa atafikishwa mahakamani leo  Jumatatu Desemba 11,2017.

Alisema kiongozi huyo alikamatwa nyumbani kwake akiwapa soda wajumbe wa UVCCM kutoka Mkoa wa Kagera kitendo ambacho ni kinyume cha maadili.

UVCCM jana Jumapili Desemba 10,2017 ilichagua viongozi wapya wa ngazi ya Taifa watakaoongoza jumuiya hiyo ya CCM kwa kipindi cha miaka mitano.

Sadifa ambaye pia ni mbunge wa Donge, Zanzibar alikamatwa nyumbani kwake Mailimbili mjini Dodoma

Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )
© Copyright MZALENDO HURU
Back To Top