Mbunge wa Singida Mashariki na Mwanasheria Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu amemshukia Spika wa Bunge, Job Ndugai kwa kutokwenda Nairobi kumjulia hali.
Ameyasema hayo wakati akifanya mahojiano
na Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC) ambapo amesema kuwa mpaka
sasa Spika wa bunge hajawahi kwenda kumtembelea.
Amesema kuwa shambulio hilo lilikuwa la kisiasa kutokana na misimamo yake mbalimbali ambayo amekuwa akiisimamia.
“Mimi ni mgonjwa wa Bunge, nikiongozi wa
Bunge, ni msemaji wa wizara ya Katiba na Sheria, ni mnadhimu mkuu wa
kambi ya upinzani bungeni, ni mtu mkubwa ndani ya bunge, mpaka leo Spika
hajaja kuniona na wala hajatuma mtu yeyote, labda wanasubiri nife ndio
waje kwenye mazishi kuniona?,”amesema Lissu
Hata hivyo, Lissu amesema kuwa mpaka
sasa bunge halijaonyesha uhusika wake katika matibabu kwakuwa halijatoa
hata senti moja kugharamia matibabu ingawa anahaki ya kupata matibabu
nje ya nchi.
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )