Naibu
Katibu Mkuu wa Chadema Zanzibar, Salum Mwalim (katikati) akitoa taarifa
hiyo. Kushoto ni Katibu Mkuu Baraza la Wazee Taifa, Roderick Lutembeka
na kulia ni Mkurugenzi wa Bunge ndani ya Chadema Halimashauri Kuu, John
Mrema.
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo
(Chadema) leo kimetoa taarifa yake juu ya utaratibu utakaotumika katika
uteuzi wa wagombea ndani ya chama hicho kwa mwaka wa 2015.
Akizungumza na wanahabari jijini Dar es
Salaam, Naibu Katibu Mkuu wa Chadema Zanzibar, Salum Mwalim ametaja
mchakato wa uteuzi kuwa utahusisha hatua tatu katika ngazi ya kata na
jimbo au wilaya na hatua moja katika ngazi ya kitaifa.
Mwalimu alisema kuwa ngazi ya kwanza ni
Mkutano Mkuu wa Jimbo ambao utafanyika siku moja kwenye eneo moja au
Makao Makuu ya Jimbo au eneo ambalo litaamuliwa na vikao vya chama,
wagombea kujipigia kura wenyewe na kamati ya utendaji ya jimbo ambayo
kazi yake itakuwa ni ya uteuzi wa awali kwa mujibu wa katiba ya chama na
kuwasilisha mapendekezo yake kwa Kamati Kuu.
Aidha, aliongeza kuwa katika utaratibu
huu wa mchakato wa kuwapata wagombea, chama hakitaingilia mamlaka
waliyojiwekea na Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) na kwa sasa tayari
wale wote wanaohitaji kuchukua fomu za kuwa wagombea, wanaweza kuchukua
katika tarehe iliyopangwa (ratiba ipo chini).
Aliongeza kuwa, fomu hizo zitaanza
kuchukuliwa katika majimbo ambayo hayana wawakilishi wao Bungeni ambapo
majimbo yenye wawakilishi, fomu zitaanza kutolewa hadi hapo Bunge
litakapokuwa limevunjwa na mchakato mzima wa utoaji fomu ukiwa tayari
umehalalishwa.
Alitaja viwango vya fomu vitakavyotumika
katika kugombea ngazi ya urais hadi udiwani kwa upande wa urais ni
Sh.1,000,000, ubunge Sh.250,000 pamoja na viti maalum. Udiwani wa kata
ni Sh. 50,000 pamoja na udiwani wa viti maalum.
Hivyo fomu hiyo itarejeshwa kwenye jimbo
au kata ambayo mgombea anagombea na ndipo atapaswa kulipia gharama za
fomu husika baada ya kuijaza na pia fomu zitapatikana katika ‘website’
ya chama ambayo ni www.chadema.or.tz
PICHA/STORI: DENIS MTIMA/GPL.
CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDEKELEO
(CHADEMA)
RATIBA YA UCHUKUAJI FOMU, VIKAO VYA UCHUJAJI NA UTEUZI WA WAGOMBEA NDANI YA CHAMA UCHAGUZI MKUU MWAKA 2015.
18/05 – 25/06/2015
|
Kuchukua na kurejesha fomu za Udiwani Kata ambazo hatuna Madiwani.
|
Makatibu Kata/Jimbo na Wilaya
|
01/7 – 10/7/2015
|
Kuchukua na kurejesha fomu Kata ambazo tuna Madiwani.
|
Makatibu Kata/Jimbo na Wilaya.
|
15/7 – 20/7/2015
|
Uteuzi wa mwisho Wagombea Udiwani Kata pamoja na wale wa Viti maalum.
|
Kamati Tendaji za Majimbo.
|
18/5 – 25/6/2015
|
Kuchukua na kurejesha fomu za Ubunge Majimbo ambayo hatuna Wabunge kwa sasa, pamoja na Fomu za Ubunge wa Viti Maalum.
|
Makatibu wa Majimbo, Wilaya, Mikoa na Makao Makuu.
|
6/7 – 10/7/2015
|
Kuchukua na kurejesha fomu za Ubunge Majimbo ambayo tuna Wabunge kwa sasa.
|
Makatibu wa Majimbo na Wilaya.
|
20/7 – 25/7/2015
|
Uteuzi wa awali wagombea Ubunge.
|
Kamati Tendaji za Majimbo.
|
20/7 – 25/7/2015
|
Kuchukua na kurejesha Fomu za Mgombea Urais.
|
Makao Makuu
|
1/8 – 2/8/2015
|
Uteuzi wa mwisho wa Wagombea Ubunge kufanyika.
|
Kamati Kuu Taifa.
|
3/8/2015
|
Baraza Kuu Taifa
|
Kamati Kuu
|
4/8/2015
|
Mkutano Mkuu Taifa
|
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )
Filed Under:
KITAIFA