Wakati Mwenyekiti wa CCM, Jakaya Mrisho Kikwete akifungua Kikao cha NEC, ametoa statement kali sanaambayo imewaacha wajumbe na butwaa kubwa. Kwa ufupi, amesema yafuatayo:

1.Chama hakitamvumilia yeyote aliyevunja na anayevunja Kanuni na hakiwezi kujifanya hamna lolote lililotokea.

2. Zama za kuamini kuwa CCM ikipitisha mgombea basi huyo ndio anakuwa Rais zimepitwa na wakati. Wana CCM ni wachache kuliko Watanzania wapiga kura. Hivyo tusichague kwa kujidanganya kwa kuwa aidha tunampenda sie au tunamuogopa. Wananchi hawatatuogopa hawatatuchagua

3. Chama hakitachagua kwa shinikizo la mtu yeyote bali kitasimamia misingi wala hakitamuogopa mtu. Chama kwanza mtu baadae.

4. Chama kinazo taarifa za wagombea Urais, waNEC na wapambe wao wanaofanya mambo ya ajabu na lazima kitachukua hatua.

5. Wananchi wana matarajio makubwa na CCM na hatuko tayari kuwaangusha.