DAHIRA
ya Isaya Mwita, Meya wa Jiji la Dar es Salaam kukamata wakwepa kodi na
kuwafikisha mahakani inatia kiwewe vigogo wengi, anaandika Happyness
Lidwino.
Amesema,
amepanga kukamilisha mambo mengi katika kipindi cha miaka mitano kwenye
nafasi hiyo lakini donda ndugu la ukwepaji kodi atashughulika nalo kwa
kuwa, limeota mizizi ndani ya jiji hilo.
Akizungumza
na mtandao huu jana Mwita ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Vijibweni
(Chadema) amesema, vigogo wakwepa kodi wanapaswa kujua kuwa “huu ni
utawala mpya wenye lengo la kurudisha maendeleo kwa watu wote bila
upendeleo.”
Amesema,
licha ya jiji hilo kuwa na vyanzo vingi vya mapato bado wananchi wake
wanaishi maisha duni kutokana na baadhi ya vigogo wenye biashara nyingi
kutolipa kodi ipasavyo.
“Nasubiri tu wiki ijayo niapishwe ili nianze kuwafuatilia wote wenye viporo vya kodi na wanaokwepa.
“Nina
mipango mingi ya kimaendeleo lakini yote inahitaji pesa ambazo ni
lazima zipatikane kwa njia ya kodi na kuongeza vyanzo vya mapato,”
amesema Mwita.
Amesema kwamba, kwa muda mrefu amekuwa akitamani kuwa meya wa jiji ili aweze kuweka wazi uozo wa utawala uliopita.
“Mimi
pia ni mmoja kati ya wananchi waliotoka katika familia ya kimaskini,
kwa hiyo ninatambua shida za wananchi ambapo nikianza kazi kwa
kushirikiana na mameya wa wilaya, zitatatuliwa,’’ amesema.
Changamoto
nyingine kubwa katika jiji hilo Mwita anataja kuwa ni uchafu
uliokithiri. “Nina mpango wa kujenga dampo kubwa kila wilaya ili kuondoa
taka zinazozagaa jijini kwa kusubiri kukusanywa na kupelekwa dampo
kubwa la pugu.
“Ninaamini kwa kufanya hivyo suala la taka kuzagaa kila mahali itakuwa ni ndoto,” amesema Mwita.
Hata
hivyo ameahidi kutatua kero ya foleni ya magari kwa kujenga maeneo ya
maegesho ya magri katika kila wilaya ili kusaidia wafanyakazi huegesha
magari yao nyumbai na kwenda katika shuguli zao kwa daladala.
Akizungumzia
uhaba wa vyoo vya umma Mwita amesema asilimia kubwa katika sehemu
muhimu zinazokaliwa na watu wengi hakuna vyoo vya bure.
“Hii
nayo ni kero kwa namna moja ama nyingine kwani vipo vya kulipia tu
hakuna vya bure na hata kama vikiwepo havina ubora. Na kuna wengine pia
hawana uwezo wa kujilipia huduma hiyo. Hili litakuwa ni jambo la haraka
kushuhulikiwa,” amesema Mwita.
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )