Featured
Loading...

Mzee wa Miaka 75 Amepigwa na Mpangaji Wake Hadi Kufa Kisa Bili ya Umeme.....


Mzee wa miaka 75 mkazi wa Ondo State nchini Nigeria, ameripotiwa kupigwa hadi kufa na mpangaji wake kisa bili ya Umeme.

Mtandao wa Naija Gists umeripoti kuwa, Baba mwenye nyumba huyo ambaye ni mstaafu wa shirika la maji Nigeria, aliwapa masharti wapangaji wake kuwa endapo bili ya umeme ikitoka basi hela ichangwe na ilipwe ndani ya masaa 24.

Taarifa inazidi kudadavua kuwa mpangaji mmoja alichelewa kutoa fedha hiyo, mwenye nyumba akaanza kumkoromea ndipo jamaa alipoamua kumshushia kipigo kilichompelekea umauti.

Mshitakiwa anashikiliwa katika kituo cha polisi cha Ondo kwa mahojiano zaidi

Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )
© Copyright MZALENDO HURU
Back To Top