Mzee wa miaka 75 mkazi wa Ondo State nchini Nigeria, ameripotiwa kupigwa hadi kufa na mpangaji wake kisa bili ya Umeme.
Mtandao
wa Naija Gists umeripoti kuwa, Baba mwenye nyumba huyo ambaye ni
mstaafu wa shirika la maji Nigeria, aliwapa masharti wapangaji wake kuwa
endapo bili ya umeme ikitoka basi hela ichangwe na ilipwe ndani ya
masaa 24.
Taarifa
inazidi kudadavua kuwa mpangaji mmoja alichelewa kutoa fedha hiyo,
mwenye nyumba akaanza kumkoromea ndipo jamaa alipoamua kumshushia kipigo
kilichompelekea umauti.
Mshitakiwa anashikiliwa katika kituo cha polisi cha Ondo kwa mahojiano zaidi
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )