Featured
Loading...

Watu 42 Watiwa Mbaroni Zanzibar Wakituhumiwa Kulipua Nyumba ya Kamishna wa Polisi

Jeshi la Polisi Zanzibar linawashikilia watu 42 wakituhumiwa kuhusika na mlipuko uliotokea juzi usiku katika nyumba ya Kamishna wa Polisi, Hamdan Omar Makame.

Akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za makao makuu ya polisi Ziwani, Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Mjini Magharibi, Mkadam Khamis Mkadam alisema hadi jana mchana watu 42 walikuwa ndani kwa ajili ya kuhojiwa na jeshi hilo.

Alisema uchunguzi unaendelea na bado watu wengine wanatafutwa kuhusiana na tukio hilo.

“Bado tunaendelea na uchunguzi wa jambo hili na tukishakamilisha tutatoa taarifa rasmi,” alisema Kamanda Mkadam.

Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )
© Copyright MZALENDO HURU
Back To Top