Featured
Loading...

Ushindi Mwingine Mnono wa Timu ya Genk Huu Hapa..Mbwana Samatta Acheza Dakika 75


Usiku wa April 20 2016 kocha wa KRC Genk Peter Maes kaendelea kumuamini na kumpa nafasi ya kuanza katika first eleven yake nahodha wa timu ya taifa ya Tanzania anayeichezea klabu hiyo Mbwana Samatta, Maes amempa nafasi Samatta ya kuanza mchezo wa pili mfululizo.

Licha ya kuwa KRC Genk walikuwa nyumbani katika uwanja wao wa Cristal Arena kukabiliana na vinara wa Ligi hiyo Club Brugge, Maes kamuamini Samatta na kumpa nafasi katika mchezo huo mgumu ulio malizika kwa KRC Genk kuibuka na ushindi wa goli 4-2. Samatta amecheza kwa dakika 75 na dakika ya 76 alitoka akaingia Nikolaos Karelis.

Samatta anakuwa amefikisha jumla ya mechi tatu alizoanza akiwa na KRC Genk katika mechi hizo amefunga mechi mbili goli moja moja katika kila mchezo, magoli ya KRC Genk ya leo yamefungwa na Onyinye Ndindi dakika ya 15, Alejandro Melero dakika ya 42, Thomas Buffel dakika ya 45 na Jeren Uronen dakika ya 73.

Kwa Sasa Genk Inashikilia Nafasi ya Nne Katika Ligi hiyo

Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )
© Copyright MZALENDO HURU
Back To Top