Msanii aliyepotea kwa kipindi kirefu na kurudi kwa style tofauti na iliyozoeleka, namuongelea Jay Moe mzee wa Pesa ya Madafu, ametoa ya moyoni kuhusu video ya ngoma yake.
Rapper Jay Moe amesema wimbo wake wa ‘Famous’ ambao alimshirikisha P-Funk, unafanya vizuri mpaka leo ukipigwa unaweza ukadhani ni mpya na hilo ndio linamfanya anajuta kwanini hakuifanyia video ngoma hiyo.
“Bado ukipigwa hadi leo unasuond wa kisasa zaidi, na kama nikisema nataka kushoot ‘kama unataka demu’ kuna wengine siwezi kuwapata kirahisi, lakini Famous it’s just me and P-Funk na kuonesha tu hiyo lifestyle ya Famous guy inakuwaje, kwahiyo tunataka tushoot hiyo,” alisema Jay Moe
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )