Najua watu wangu wa nguvu wanaopenda
soka la ulaya, huu ni wakati ambao wanafuatilia kwa karibu mipango na
uboreshwaji wa timu wanazozishabikia, headlines za usajili wa wachezaji
soka ndio zinatawala kwa sasa, najua utakuwa ulisikia stori za Alex Sanchez wa Arsenal kuhusishwa kujiunga na Juventus ya Italia.
Mkurugenzi wa klabu ya Juventus ya Italia Giuseppe Marotta ameamua kuweka wazi ukweli kuhusiana na stori hizo za Juventus kumuhitaji Sanchez, Marotta amesema ni kweli Juventus wanamuhitaji Sanchez lakini wanajua haiwezi kuwa rahisi kwa Arsenal kumuachia nyota huyo ajiunge nao.
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )