Featured
Loading...

Kijana apachikwa jina ‘Mkereketwa wa Mwendokasi’ baada ya kumfanyia Rais Magufuli kitendo hiki


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli hivi karibuni katika ziara zake alikutana na kijana aliyemshangilia kwa nguvu zake zote hali ambayo ilimfanya mkuu huyo wa nchi kumwita na kupiga naye picha.

Kijana huyo ambaye anaitwa Omar Abdalah Ramadhani ‘Mkereketwa wa Mwendokasi’ alisikika akisema “Magufili kule aliko, aminia mzazi, Mungu akupe baraka zote mzazi, na asiyekupenda Mungu atamtokomeza, Watanzania tuko nyuma yako” kauli iliyomfanya Rais Magufuli amwite ili apige naye picha na baadaye kuombewa dua na kijana huyo.

Baada ya tukio hilo kufanyika na kurekodiwa, kijana huyo anaendelea kuwa maarufu katika mitandao ya kijamii huku baadhi ya watu wakiwa amepachikwa jina la ‘Shabiki wa Mwendokasi’

Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )
© Copyright MZALENDO HURU
Back To Top