Featured
Loading...

Mr Blue: Barakah na Naj Walitaka Kunivunjia Ndoa Yangu


Mr Blue amekiri kuwa skendo yake kuwa amekuwa akiwasiliana na ex wake, Naj ambaye kwa sasa ana uhusiano na Barakah Da Prince ilitaka kuivunja ndoa yake.

Akiongea na Clouds FM, rapper huyo wa ‘Mboga Saba’ amedai kuwa mke wake, Wahyda sasa amekuwa na wivu wa kufa mtu tangu kuzuke skendo hiyo.

“Sasa hivi naona kama wivu umezidi baada ya hii skendo ya hawa jamaa kuitengenezea kiki kwasababu wanataka kutoa nyimbo yao, skendo kwamba mimi nilimpigia yule mwanamke mwingine nani anaitwa, Najma yule. Wametengeneza kweli kabisa, mimi nimezipata za kunyapianyapia kwamba wametengeneza ili kukikisha nyimbo zao,” amesema Blue.
“Lakini wamenikosea sana kwasababu wanataka kugombanisha ndoa yangu, mimi nina mke ujue, siwezi kumpigia mtu ambaye nimemwacha, ni kosa kubwa sana, halafu mke wangu yule ni mwanamke ambaye walikuwa watatu kupigania nani awe na mimi, yaani bora hata ningempigia mtu mwingine,” amesisitiza.

“Ilifika karibu kama siku mbili tuna ugomvi mimi na mke wangu, ni kitu kikubwa sana, nimekasirika sana, nimechukia sana na nawaambia mashabiki wangu, alichokifanya Barakah na watu wake, kama sio yeye simlaumu, kama watu wake nilikuwa naomba waoneshe proof kwenye mitandao waoneshe namba yangu niliyompigia, waioneshe kwamba ni hiyo kweli sio unaongeaongea tu.”

Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )
© Copyright MZALENDO HURU
Back To Top