Featured
Loading...

Aliyecopy Hotuba ya Obama na Kumpa Rais Buhari…Kufukuzwa Kazi


Wiki iliyopita Ikulu ya Nigeria kupitia kwa muandishi wa hotuba za Rais, iliingia kwenye skendo ya kunakili hotuba ya Rais Barack Obama na kumpa Rais wa Nigeria, Muhammadu Buhari ambaye aliisoma kama ilivyo bila kujua, mpaka wapinzani walipoanzisha mzozo juu ya suala hilo.

Official responsible for Plagiarism of Obama's Speech to be sacked

Sehemu ya hotuba ya Rais Buhari iliyonakiliwa kutoka kwenye hotuba ya Rais Barack Obama aliyoitoa mwaka 2008 inasema “Change Begins With Me” Mabadiliko Huanza Na Mimi, ikifahamika kwa jina la Hotuba ya Ushindi.

Ikulu ya Nigeria imeomba radhi juu ya aibu iliyomkuta Rais wa nchi hiyo na kuahidi kumchukulia hatua kali za kinidhamu muandishi aliyesababisha.

Kwa mujibu wa gazeti la Daily Trust limesema kuwa kiongozi huyo msaidizi wa idara ya mawasiliano ya Rais, ataondolewa kazini kutokana na uzembe alioufanya. Muda mfupi tangu kutokea tatizo hilo, Taasisi ya Rais kupitia idara ya mawasiliano kwa Umma imeripoti kuwa itaweka software itakayokuwa ikigundua kama hotuba zote za Rais zimenakiliwa kutoka sehemu nyingine.

Msemaji wa Serikali ya Nigeria amesema >>>Tumepanga kuchukua hatua ya kuweka kifaa kitakachokuwa na uwezo wa kukagua na kugundua kama hotuba za Rais zimenakiliwa kutoka sehemu nyingine kabla ya kumkabidhi Rais,”

Kitendo cha Hotuba ya Rais Buhari kunakiliwa kutoka kwenye Hotuba za Rais Obama, kimewafanya vyama vya upinzani nchini humo kusema kuwa ipo siku Rais huyo atasaini nakala za kujiuzulu bila kujua kutokana na kutozikagua kabla ya kuzisoma.

Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )
© Copyright MZALENDO HURU
Back To Top