Aliyekuwa 
 Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. 
Willibrod Slaa, ameajiriwa katika duka kubwa la bidhaa za majumbani 
(Supermarket) la Costco lililopo Oakville, Toronto nchini Canada, 
imebainika.
Dk. Slaa, kwa sasa anaishi nchini Canada alikokwenda kwa masomo, tangu alipotangaza kuachana na siasa Septemba 1, mwaka 2015.
Kwa
 muda wa wiki kadhaa, ziliibuka taarifa katika mitandao ya kijamii kuwa 
mbunge huyo wa zamani wa Karatu, amemaliza masomo yake na sasa anafanya 
kazi katika moja ya maduka makubwa ya bidhaa mbalimbali nchini humo – 
Supermarket.
Supermarket
 ya Costco anayofanya kazi Dk. Slaa akihudumu kama Mshauri wa Mauzo 
(Sales Advisor), akilipwa Dola za Marekani 10 (zaidi ya Sh 20,000) kwa 
saa, ina hadhi kama Nakumat, Shopers, Imalaseko, Game na maduka mengine 
makubwa nchini.
Akizungumza
 na Gazeti la Mtanzania jana kwa simu , Dk. Slaa alisema kuwa kwa sasa 
anaishi kwa kazi ya mikono yake  kwani ili aweze kuishi anahitaji 
kufanya kazi zaidi ya mbili hadi nne kwa siku.
“Niko,
 ninafuatilia matukio Mutukula (ziara ya Rais Dk. John Magufuli jana). 
Siku zote nimesema ninaishi kwa jasho na kazi ya mikono yangu. Canada 
ili uishi vizuri, unahitaji kazi zaidi ya mbili au tatu mpaka nne. Hayo 
nimeweka wazi, sijui jambo jipya kama mtu alikuwa hafuatilii.
“Mimi
 ninafanya kazi PWD/CDS/COSTCO kama Sales Advisor, baada ya kumaliza 
masomo yangu hasa Interpersonal Communication. Costco ninakofanya kazi 
ina members (wanachama) 10,000.  Kwa siku wanaofika Warehouse ni kati ya
 5,000 hadi 7,000,” alisema Dk. Slaa.
Mbali na hilo, alisema kuwa pia anafanya kazi nyingine ikiwa ni pamoja na ushauri (Consultancy).
Alisema
 kila mara amekuwa akiwataka Watanzania na vijana wafanye kazi kwani 
fedha haziji kwa kukesha kwenye mtandao wala propaganda.
“Canada
 ni kazi, Profesa wa Chuo Kikuu anafanya kazi ya Uber. Sijui kama Uber 
inafahamika Tanzania, ni dereva Taxi kwa kutumia gari lake binafsi. 
Ofisa wa Serikali usiku anaosha vyombo hotelini.
“Ndiyo
 maana familia ina magari mawili au zaidi, TV, nyumba ya kisasa, chakula
 cha kisasa. Wanatekeleza sera ya ‘Hapa Kazi Tu’ kwa matendo. Nadhani 
nimekupa taarifa za kutosha ikiwa ni pamoja na kujibu propaganda kuwa 
nilihongwa mabilioni.
“Niwahakikishie
 tena, wakati wa kusoma nilikuwa na scholarship, tangu nianze kazi 
ninaishi kwa jasho la mikono yangu. Mke wangu yeye ameingia Chuo Kikuu 
cha York baada ya Diploma yake na bado anapata scholarship.
“Ndiyo
 maana tuna uwezo wa kuwa na magari mawili aina ya Jeep na Dodge, 
ukifanya kazi utaishi vizuri. Hii ni pamoja na kugharamiwa bima ya afya 
(Health Insurance), watoto kusomeshwa na Serikali ya Canada,” alisema 
Dk. Slaa.
Mei
 mwaka huu, Dk. Slaa, alisema hana mpango wa kurudi nchini kwa sasa na 
kwamba taarifa zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii hazina ukweli 
wowote.
Hata
 hivyo, Dk. Slaa ambaye alipata kuwa Mbunge wa Karatu kwa vipindi vitatu
 mfululizo, hakuweza kuainisha mazingira yaliyomfanya aondoke nchini na 
kwenda kuishi ughaibuni.
Septemba,
 2015 wakati wa Uchaguzi Mkuu, Dk. Slaa alijiweka kando na siasa, kwa 
kile alichokieleza kutofautiana na viongozi wenzake ndani ya chama chake
 juu ya masharti ya kumpokea aliyekuwa mgombea urais wa Umoja wa Katiba 
ya Wananchi (Ukawa), Edward Lowassa.
“Sina
 tabia ya kuyumbishwaa, sina chuki na mtu yeyote, sipendi siasa za 
udanganyifu na propaganda. Nimeachana na siasa tangu Julai 28, 2015, 
baada ya kuona misingi ya chama nilichoshiriki kukijenga imepotoshwa,” 
alisema Dk. Slaa siku alipotangaza kuachana na siasa.
Alisema
 sharti la kwanza ambalo alitaka Chadema izingatie, ni kiongozi huyo wa 
zamani ndani ya Serikali ya CCM, kujisafisha dhidi ya tuhuma ya kashfa 
ya sakata la Kampuni ya Kufua Umeme ya Richmond aliyohusishwa nayo akiwa
 Waziri Mkuu.
Credit: Mtanzania 
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )
 

 
 
 
 
 
 
 
