Serikali
 inatarajia kuanzisha mfumo mpya wa elimu hapa nchini ambao elimu ya 
msingi itakuwa inatolewa kwa miaka 6, tofauti na ilivyo sasa ambapo 
hutolewa kwa miaka 7.
Akijibu
 swali linalohusu watoto wa kike kuolewa wakiwa na cheti cha kuhitimu 
elimu ya sekondari, Naibu Waziri wa TAMISEMI Mheshimiwa Joseph Kakunda 
ametolea ufafanuzi suala hilo na kusema kwamba mfumo huo mpya utatoa 
fursa kwa wanafunzi wa elimu ya msingi kusoma miaka 6, huku chekechea 
ukiwa ni mwaka mmoja na sekondari ni maka minne, ambayo itakuwa ni 
lazima.
“Napenda
 kutoa majibu sahihi waliopata mkanganyiko, nilisema sera mpya ya elimu 
huko tunakoelekea inabadilisha mfumo wa sasa wa elimu ambao utahitaji 
mtoto aanze chekechea mwaka mmoja, elimu ya msingi miaka 6, sekondari 
miaka minne na itakuwa ni lazima”, amesema Mheshimiwa Kakunda.
Mheshimiwa
 Kakunda ameendelea kwa kueleza kwamba kutokana na mfumo huo mpya ambao 
utaruhusu mwanafunzi kusoma kwa muda mfupi, na baada ya kuhitimu ndio 
utakuwa kithibitisho pekee kwamba binti amemaliza elimu ya sekondari na 
ndipo ataruhusiwa kuolewa.
Hivi
 karibuni Waziri kakunda alitoa taarifa ikisema kwamba ili mtoto wa kike
 aweze kuolewa atahitaji kuwa na cheti cha kuhitimu sekondari, suala 
ambalo liliibua mjadala kwa wananchi.
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )
 

 
 
 
 
 
 
 
