Featured
Loading...

Siri Ya Bundi Kupendwa Na Wachawi

Wakati  watu wengine  wakimuona  bundi  kama  ishara  ya  uchuro, nuksi  na  mikosi, wachawi wao  humuona  bundi  kama    kiumbe  mwenye hekima  na  busara.

Haya  si  maneno yangu  bali  ni  maneno  ya Mganga wa  Jadi kutoka  nchini  Tanzania  ajulikane  kama  MUNGWA  KABILI.
 
Dokta. MUNGWA  KABILI aliyasema  maneno  hayo  hivi  karibuni, alipokuwa  akifanya  mahojiano  ya  moja  kwa moja  kwenye  kituo  kimoja  cha  redio  kilichopo  jijini  Mombasa  nchini  Kenya.
 
Maneno ya  Dokta Mungwa  yalikuja mara  baada  ya  mwanamama  mmoja  kutoka  Malindi  Kenya  kupiga  simu  akielezea  alivyo  jawa  na  hofu  kubwa  kwa  sababu  usiku  wa  kuamkia  siku  hiyo,  bundi  walitua kwenye  mti  ulio kuwa  kwenye  nyumba  iliyo  jirani  yake  na  kutoa vilio  vya  uchuro  kwa  masaa  mawili.
 
Dokta  Mungwa  Kabili  alikuwa  na  haya  ya  kusema :
Pole  sana  dada  angu  kwa  masaibu  yaliyo  kukuta, lakini  hata  hivyo  usiwe  na  hofu  kwa  sababu, si kila  mlio  wa  bundi  una  maanisha  uchuro.  Wakati  mwingine  bundi  hutoa  sauti  kumaanisha  kitu  tofauti  kabisa  lakini  kwa  sbabu  watu wengi  tumeshajiaminisha  kuwa  kila  bundi  aliapo ni  uchuro  basi  tunapotokea  na  hali  hiyo  hujawa  na  hofu  kama  ilivyo  kutokea  wewe.
 
Kitu  kimoja  cha  hakika  ninacho penda  kukujulisha  ni  kwamba,  siku  yoyote  utakayo  pata  kusikia  sauti  ya  bundi,  basi  jua  kuwa  umesikia  sauti  hiyo  kwa  sababu  bundi  wenyewe  ndio  wametaka  wewe  usikie  sauti  yao. Hii  maana  yake  nini  ? Maana  yake  ni  kwamba, kuna  ujumbe  ama  ishara  fulani  ambayo  bundi  wanataka  uipate.
 
Katika  ndege  wote  walio umbwa  na  Mwenyezi  Mungu, bundi  ndio  ndege  pekee  mwenye  uwezo  wa  kuruka,kupaa  na  kutua  bila  kupiga  kelele wala  kutoa  sauti  yoyote  ile. Mungu  ameya  dizaini  mabawa ya bundi katika namna  ya  kipekee, namna  inayo  mfanya  bundi  aweze  kupaa  bila  kupiga  kelele  pamoja  na  kwamba, kwa kufanya  hivyo  huku’nguta  mbawa  zake.
 
Bundi  anaweza  kutua  kwenye  paa la nyumba  yako, akakaa  hadi alfajiri  na  kuondoka pasi na  wewe  kujua.
Ukiona  umesikia  sauti  ya  bundi, basi  tambua  ni  bundi  mwenyewe  ndio  amekusudia  usikie  sauti  yake  kwa sababu  kuna  ujumbe  maalumu  anataka  kukupa.
 
Wachawi  wanamfahamu  vizuri  sana  bundi  ndio  maana  wanampenda  sana  wala  hawashitushwi  na  mlio  wake.
Wachawi  wanampenda  sana  bundi  kiasi  cha  kuiga  karibu  tabia  zote  za ndege  huyu  wa usiku.

Baadhi  ya  tabia  za  bundi  ambazo  wachawi  wameziiga  ni  pamoja  na:

1. Bundi ndio ndege  pekee  ambae  huwa  hapigi  kelele  anapokuwa  anapaa  na  kutua. Ndege  wengine  wote  huwa  wanapiga  makelele  pindi  wanapokuwa  wanapaa  kwa  sababu  ya  kupiga  mabawa  hali  ambayo  ni  tofauti  kwa  bundi. Bundi  hupaa kimya  kimya  na  hutua  kimya  bila  mawindo  yake  kujua.  Hii  inatokana  na  jinsi  Mungu alivyo  ya  dizaini  mabawa  na  manyoya  yake  ili  viweze  kumsaidia  kupata  ridhiki yake  ya  kila  siku. Wachawi  wanapokuwa  wanafanya  mipango  yao  ya  kichawi  hufanya  kimya  kimya  bila  watu  wengine  kujua. Na  huwa  hawataki  kabisa  kujulikana.

2. Bundi  hutaka  sauti  yake  isikike  pale  tu  anapo  amua  isikike.  Unaposikia  sauti  ya  bundi  jua  umeisikia  kwa  sababu  ametaka  uisikie  na  wala  si  vinginevyo . Vivyo hivyo  wachawi  pia  hutaka  nguvu  zao au  mambo  yao   yajulikane  pale  tu  wanapotaka  vijulikane  na  si  vinginevyo.

3. Bundi  huanza  kuruka  usiku giza  linapo  ingia. Vivyo  hivyo  wachawi  huanza  shughuli  zao usiku  pindi  giza  linapo  ingia.

4. Sio kwamba  bundi  hawawezi  kuruka  mchana . Wakati mwingine  bundi  huruka  mchana  kutafuta  mawindo  yao  na  hufanya  hivyo  pindi  kunapo kuwa  na  sababu  ya  msingi kama vile  kutafuta  chakula  hasahasa  katika  kipindi  ambacho wanakuwa na   upungufu  wa  chakula  au  hawakupata  mawindo  ya kutosha  wakati  wa  usiku.

Vivyo  hivyo  wakati  mwingine  wachawi  hulazimika  kufanya  baadhi  ya shughuli  zao  nyakati  za  mchana  ingawa  uchawi  unao  fanyika  usiku  huwa  na  nguvu  kubwa  zaidi  kuliko  unao  fanyika  mchana.

5. Bundi  hupenda  kufanya  shughuli  zao  usiku  wakati  mawindo  yao  yamelala, vivyo  hivyo  wachawi  hupenda  kufanya  shughuli  zao  usiku  wakati  wahanga  wao  wamelala.

6. Bundi  huwa  hawajengi  vichali  vyao  wenyewe  na  badala  yake  hutumia  vichali  vya  ndege  wawindao  mchana  kama  vile  mwewe,  fundi chuma  na  kunguru.    Vivyo  hivyo  wachawi  huwa  hawaishi kwenye  nyumba  walizo jenga kwa  jasho  lao  wenyewe. Huishi  kwenye  nyumba  zilizo  jengwa  na  watu  wengine, na  wao  huzimiliki  kwa  kutumia  nguvu  ya  uchawi.

Kama  hiyo  haitoshi ,wachawi   huwa  hawahifadhi  majini  wabaya  kwenye  miili  yao  wenyewe. Hutumia  miili  ya  watu  wengine  kuhifadhi  majini  na  mapepo  wachafu. Wakati mwingine  unaweza  kuwa  na  mapepo  wachafu  sio  kwa  sababu  kuna  watu  wamekutumia  ili  upate  madhara  ila  kwa  sababu  wachawi  wanatumia  mwili  wako kama  kibanda  cha  kufugia  na  kutunzia  majini  yao.

7.  Wakati mwingine   bundi  hulana  wao kwa  wao.  Bundi  wakubwa  wenye  pembe  kubwa  huwala  bundi  wa  saizi ya  kati  na  bundi  mbilikimo  vivyo  hivyo  bundi  wa  saizi  ya  kati  hula  bundi  mbilikimo isipokuwa  bundi  mbilikimo ndio  hawana  uwezo  wa  kuwala  bundi wengine.  Vivyo  hivyo  wachawi  hutoa  sadaka  zap  watoto  wao , waume,wake , wazazi  na  ndugu  zao.

8.  Kwa kawaida  bundi  huishi  hadi  miaka  kumi . Bundi  hutaga  mayai  matatu  hadi  manne na huatamia  mayai  kwa  wiki tatu  hadi  nne.  Wanapototoa  watoto, bundi  mbilikimo  huwalisha  makinda  yao  kwa  siku  27  wakati  bundi  wa  saizi  ya  kati  na  wale bundi wakubwa wenye mapembe  makubwa  huyalisha  makinda  yao kwa  muda  wa  siku 70. Wanapokuwa  wanayalisha  makinda  yao, huyalisha  kwanza  makinda  yenye  afya  na  nguvu  kisha  hufuata  makinda  dhaifu. Hii  maana  yake ni  kwamba, kama  hakuna  chakula  cha  kutosha, basi  makinda  yaliyo  dhaifu  yatakufa   kwa  njaa.  Vivyo hivyo  wachawi katika  kafara  zao  huwa  wanatoa  kafara  zilizo  nona  kwanza  kisha  hufuata kafara  dhaifu.

9. Bundi  hawaoni  vitu  vya  karibu, huona  vitu  vya  mbali tena  mbali  sana. Vivyo hivyo   Wachawi  kwa  kutumia  rada  zao  za  kichawi  wanaweza  wasijue  kesho  utapatwa  na  nini  lakini  wanaweza  kujua  utakuja  kuwa  nani  baada  ya  miaka  ishirini ijayo.  Ndio  maana  huweza  kuiba  nyota  za  watu wakingali  wachanga.

10. Ukiachilia  mbali  nyani  na  sokwe, bundi  ndio  kiumbe  mwenye  sura  inayo  fanana  sana  na  sura  ya  mwanadamu.   Hii  ni  kwa  sababu  macho   ya  bundi  yamekaa  kama ya  mwanadamu. Macho  ya  bundi  yamekaa   kwa  mbele  na  yanaona  kitu  kimoja  kwa  wakati  mmoja   ilihali  ndege  wengine  macho  yao  yamekaa  pembeni  kulia  na  kushoto   na yanaona  vitu  viwili  kwa  wakati  mmoja, yani  jicho  la  kulia  linaona  kitu  kingine  na  jicho  la  kushoto  linaona  kitu  kingine  kwa  wakati  mmoja.

Kwa  sababu  hii  Mungu  amempa  bundi  shingo  yenye  uwezo  wa  kuzunguka  mbele  nyuma . Unapopita  kwenye  mti  ambao  bundi  ametua  atakutazama, ukimpita  katika  usawa  wake  wa  machoi  atageuza  macho  yake  na  kukutazama  hadi  mwisho  wako. Wachawi  pia  hufanya  vivyo  hivyo.  Unapowapita  katika  vijiwe  vyao,watakutazama  hadi  utakapo  malizikia.

11. Bundi  hufumba  macho  kama  mwanadamu  yaani  kutoka  juu  kwenda  chini  tofauti  na  ndege  wengine  wote  ambao  wao hufumba  macho  kutoka  chini  kwenda  juu.

 Na Sio kweli  kwamba  bundi  hawaoni mchana, bundi  wanaona  mchana  vizuri  sana  tu, ila  kwa  sababu  macho  yao  ni  makubwa na  makali  sana  yenye  uwezo  wa  kuona mara  saba  zaidi  ya  mwanadamu, usiku kwao  huwa  kama  mchana  kwetu  ndio  maana  hupendelea zaidi kuwinda  usiku.  Wachawi  hutoka usiku  kuwanga  sio  kwa  sababu  hawaoni  mchana. Hufanya  hivyo  kwa  kumuiga  bundi.

12.Bundi  anapokutana  na  hatari  hutuna  na  kuwa  mkubwa  mara  mbili  ya  ukubwa wake  wa  asili. Mchawi  anapokutana  na  changamoto   yoyote katika  shughuli  zake  za  kichawi   huenda  kutafuta  msaada  kwa  wachawi  wenye uwezo  mkubwa  mara mbili zaidi  yake.

13.Bundi  huwa  na  mkia  mfupi  sana  kiasi  kama  huwajui  bundi  ukimuona  kwa  ukaribu  zaidi  kwa  mara  ya  kwanza  unaweza  kudhani  mkia  umekatwa. Wachawi  huwa  na  mawazo  mafupi sana. Mfano Wachawi  hutumia  mkia  wa  bundi  kufanya  shughuli  mbalimbali  za  kichawi  kama vile  kufupisha  maisha  ya  maadui zao, au  kufunga  maumbile  ya  kiume  yawe  mafupi, kufunga  mahusiano yawe  mafupi nakadhalika.

14. Pamoja  na  kwamba  bundi  wana  tofautiana  ukubwa  wa  maumbile, yaani  wakubwa, saizi ya  kati  na  wadogo  ama  bundi  mbilikimo, lakini  bundi  wote wana  sifa  zinazo  fanana,  mfano  bundi  wote  huwa  na  vichwa  vikubwa  kuliko  maumbile  yao, wote wana  manyoya  laini, wote  huwa na   mikia  mifupi  sana, wote  huwa  na  rangi  ima  ya  kahawia  au  ya  kijivu , huwa  na  milio  inayo  fanana, huruka  na  kupaa  kimya kimya, huwa  na  manyoya kwenye  miguu. Vivyo  hivyo  wachawi  pamoja  na  kwamba, wanaweza  kuwa  na  nguvu  na  madaraja  tofauti  katika  uchawi,lakini  wote  huwa  na  tabia  zinazo  fanana  kama  vile  chuki, husda, unafiki , roho ya  mbaya,mawazo mafupi  nakadhalika.

15. Pamoja  na  kwamba  bundi  wote  huanza  kutafuta  mawindo  yao pindi  giza  linapoingia, lakini  hutoka  kwa  nyakati  tofauti  tofauti.   Mara  nyingi  huanza  kutoka  bundi  mbilikimo. Hawa  bundi  mbilikimo  hasa  wale  wanaoishi  porini hutoka  kuanzia  saa  4 usiku, bundi  wa  saizi  ya  kati hutoka  kuanzia  saa  sita  usiku  na  bundi  wenye  pembe  kubwa  hutoka  kuanzia  saa  nane  za  usiku .  Wachawi  nao  wanapo  kuwa  wanaenda  kuwanga  na  kufanya  shughuli  zao  za  kichawi  nyakati  za  usiku  hupishana  nyakati. Ingawa  vikundi vingi  vya  kichawi  huanza  kutoka  kuanzia  saa  sita  usiku,  lakini  hupishana. Vingine  hutoka  saa saba , vingine  saa  nane. Tofauti  ni  kwamba  karibu  wachawi  wote  hurudi  majumbani mwao  nyakati  sawa.

Hata  hivyo, bundi  hutoka  kwa  nyakati  tofauti  kwa  sababu  maalumu.  . Bundi  karibu  wote  wakubwa  kwa  wadogo  hushea  vichali na huishi  katika  eneo moja.  Hutoka  kuwinda  nyakati  tofauti  tofauti kwa  ajili  ya  kupunguza  ushindani  wakati wa  mawindo..
 
16. Pamoja  na  kwamba  macho  ya  bundi  yana  nguvu  sana  lakini  wanapokuwa  katika  mawindo  hutumia  zaidi  masikio  yao  kuliko macho  yao.  Masikio  ya  bundi  yana  nguvu  sana  na  huweza  kusikia  hata  sauti  ya  kitu  kilicho  umbali  mrefu  sana. Hata hivyo  bundi  wanapokuwa  wanaenda  kuwinda  wakati  wa  mchana  hutumia  macho  zaidi  kuliko  masikio.  Vivyo  wachawi, huamini  zaidi  vitu  wanavyo visikia  kuliko  wananvyo  viona. Yaani  mchawi kila anacho  ambiwa  kuliko  kile  alicho  kiona. Kwa mfano   wewe  A  una  ujauzito hata  wa  miezi sita. Lakini kwenye  kilinge  cha  wachawi  alipoenda  kukuroga ,ukapewa  jina  kuwa  wewe  ni  MGUMBA. Basi  mchawi  ataendelea  kukuita  na  kukuchukulia  na kuamini  kuwa  wewe ni  mgumba. Ataendelea  kuamini  hivyo  hata  kama  utazaa watotyo  kumi.

17. Bundi  wanapokuwa  wanapaa  huutawala  upepo  na anga. Wana  mamlaka  juu  ya  anga , na upepo. Vivyo wachawi  wanapo  kuwa  wanapaa  huamini  kuwa  wana  mamlaka  juu  ya  anga  na  upepo  kama  alivyo  bundi.

18.  Bundi  huzungusha  kichwa  kupima  umbali  wa  anapotaka  kuruka  vile vile  wachawi  hupima nguvu  ya  kiroho  ya  mtu kabla  ya  kumtupia  uchawi.

19. Ukiachilia  mbali  bundi  wanao  kula  wadudu, bundi  wengi  huwa  hawana  tabia ya  kuhama  hama. Wanaweza  kukaa  katika  eneo  moja  kwa  zaidi  ya  mwaka  mmoja. Wachawi pia  huwa  hawami hami. Huweza  kukaa  katika  mtaa  mmoja  kwa  zaidi  ya  miaka  arobaini. Na  wanapokuwa  wanatengeneza  uchawi  wa  kuwatuliza  wanaume  kimapenzi  hutumia  vichali  vya  bundi walio  kaa  kwenye  kichali hicho  kwa  muda  wa  mwaka  mmoja  na  zaidi.

20. Wakati  mwingine  bundi  hupenda  kuwinda  wadudu  wanao  tembea  usiku  ili  kuwa  na  uhakika  wa  kupata  kitoweo.  Wadudu  hao  ni  popo.  Vivyo  hivyo  wachawi wakati mwingine  hufanya  ulozi  nyakati  za  usiku   katika  maeneo  au  mazingira  ambayo  walengwa  wao  wanakuwa  macho  ili  kuwa  na  uhakika  wa  kupata  mawindo  yao.  Mfano  ni kwenye  klabu  za  usiku zinazo  kesha,  kwenye  misiba  au  sherehe  zinazo  kesha  nakadhalika

21.   Tunafahamu  kuhusu  uwepo  wa  bundi  pindi wanapo  toa  milio  na  sio  pindi wanapokuwa  kimya.  Vivyo tunafahamu  kuhusu  uwepo wa  wachawi  katika  mazingira  tunayo  ishi  pindi  wanapo  tupa  uchawi  wao na  sio  wanapokuwa  hawajatupa  uchawi.

22.              Bundi  wakubwa  hutoa  sauti  kubwa  kuliko  bundi  wadogo. Vivyo  hivyo, wachawi  wadogo  hujulikana  zaidi  kuliko  wachawi  wakubwa.

KWANINI  WACHAWI WANAMPENDA  SANA  BUNDI
Wachawi  wanampenda  sana bundi  kwa  sababu   wana  amini  bundi  ni  kiumbe  mwenye  faida  nyingi  sana  kwao.    Baadhi  ya  mambo  ambayo  wachawi  huya  amini  kama  faida  zinazo letwa  na  bundi  ni  kama  ifuatavyo :

1.Bundi  huwasaidia   wachawi  kuchunga  misukule  yao  ; Katika ulimwengu  wa  wachawi  mtu  aliye  chukuliwa  msukule  mara  baada  ya  kukatwa  ulimwi  hatua  inayo  fuatwa  huwa  ni  kulishwa  vumbi  la  mifupa iliyo  temwa na  bundi.   Dawa hiyo  huufanya  msukule  huo  usahau  kila  kitu  ulichokuwa  unakijua  kabla  ya  kuchukuliwa  msukule.

Kwa  wasio  fahamu, bundi  huwa  wanakula  wadudu  na  wanyama  mbalimbali  kama  vile  nyoka, nge,panya, pimbi, panyabuku, ndezi,  popo  na hata  samaki.  Bundi  huwa  wanakula  vitu  vizima  vizima  na  kutema  mifupa  yao. Sasa  hii  mifupa  inayo temwa na  bundi  ndio  wanayo  itumia  wachawi  kuwalisha  misukule   wao  kwa  minajili  ya  kuwafanya  wasahau  kila  kitu  walichokuwa  wanakijua  kabla  hawaja  chukuliwa  msukule  pamoja  na  kuwapa uwezo  wa  kuona  mambo  yasiyo  onekana  na  kutokuonekana na  watu  wa  kawaida.
2. Bundi  huwasaidia  wachawi  kulinda  mashamba  yao  dhidi  ya  wadudu  waharibifu  wa  mazao

Moja kati  ya  shughuli  kuu  za  wachawi  ni  kilimo  kwa  kuwatumia  misukule. Kwenye  mashamba  huwa  kunakuwaga  na  panya  waharibifu  wa  mazao . Na  kama  nilivyo  sema  hapo  mwanzo  kuwa,  moja  kati  ya  yakula  vinavyopendwa  sana  na  bundi  ni  panya.  Kwa  wastani  bundi mmoja  anaweza  kula  hadi  panya  elfu  moja  kwa  mwaka.  Mchawi  akiwakaribisha  bundi  ishirini  kuwa  wanatembelea  kila  siku  shambani  kwake  maana  yake  ni kwamba  ndani  ya  mwaka  mmoja  watakuwa  wamemsaidia  kula  panya  elfu  ishirini  ambao  wanaweza  kuharibu  hadi  tani  31  za  mazao.

Hivyo  basi  kwa  wachawi  hapo  bundi  huwa  msaada  wao  mkubwa  wa  kiuchumi. Huwasaidia  kutunza  na  kulinda  mashamba  yao  dhidi  ya  wadudu  waharibifu. Huwasaidia  kuokoa  gharama  za  kununua  dawa  za  kuua  wadudu  waharibifu  ambazo  zingeweza  kuwagharimu  mamilioni ya shilingi.

3.Bundi  huwasaidia  wachawi  kuondokana  na  madhara  ya  wadudu  hatari  kama  nyoka na  nge

Bundi  ni  walaji  wazuri  sana  wa  wadudu  hatarishi  kwa  binadamu  kama  vile  nyoka na  nge. Hivyo  kwa  mchawi  kuwakaribisha  bundi  shambani kwake  au  nyumbani  kwake  anakuwa amejihakikishia  kuwa  hawezi  kupatwa  na madhara  ya  kuumwa  na  nyoka  au  nge  kwa  sababu  bundi  wanapoweka  makazi  yao katika  eneo  lolote  lile, nyoka  hawawezi  kukaa  mahali  wapo.
4. Bundi  huwasaidia  wachawi  katika  shughuli  mbalimbali  za  kichawi.

Kwa  kutumia  maarifa  ya  kichawi, wachawi  humtumia  bundi  katika  shughuli  mbalimbali  zap  kichawi  kama  vile :

i.           Kwenda  kuzimu  :  Bundi  ni  mesenja  wa  kuzimu  na  dunia. Huchukua  habari  za  kuzimu  na  kuzileta  duniani na   habari  za  duniani  huzipeleka  kuzimu .  Bundi  ni  daraja  linalo  unganisha  kuzimu  na  duniani. Ni daraja  linalo  unganisha  ulimwengu  usio onekana  na  ule  unao  onekana.   Kwa  wale  wasio  fahamu, umbali  kutoka  duniani  na  kuzimu ni  kilomita  sifuri. Moja  kati  ya  mawakala  wa  malango    makuu  yanayo  unganisha  dunia  na  kuzimu  ni  huyu ndege  aitwae  bundi.Ukaribu  na  urafiki  wa  wachawi  kwa  ndege  huyu  unawanufaisha  wachawi na  kuzimu

ii.         Kuiba  na  kuharibu  nyota  za  watu  hususani  watoto  wachanga :   Wanapokuwa  katika  mchakato  wa  kuiba  nyota  za  watu  hususani  watoto  wachanga,  wachawi  humtumia  bundi  kufanikisha  mchakato.

KWANINI  WANAMTUMIA  BUNDI : Bundi   ana  sifa  moja  kubwa  sana. Hana  uwezo  wa  kuona  vitu  vya  karibu lakini  ana  uwezo  wa  kuona  vitu  vya  mbali  sana.  Hiyo  ni sifa  yake katika  ulimwengu wa  nyamja  ambayo  ina  sadifu  sifa  na  uwezo  wake  katika  ulimwengu  wa  roho. Katika  ulimwengu  wa  roho  bundi  ana  uwezo  wa  kuona  na  kujua  mambo  yatakayo  mtokea  mtu  miaka  30  hadi  sitini  ijayo. 
 
Bundi  anaweza  kuona  kifo  cha  mtu  miaka  kumi  mbele, siku moja  mbele, siku mbili  mbele, wiki nakadhalika.
Hii ndio  sababu  inayo  mfanya  bundi  kutoa  taarifa  kwa  mhusika, ndugu, jamaa  na  marafiki  zake siku kadhaa  kabla  ya  kifo  cha  mtu  huyo.
 
Bundi  hufanya  hivyo  kwa  kutoa  mlio maalumu. Wachawi  kwa  sababu  wanafundishwa  namna  ya  kuwasiliana  na  bundi, bundi  anapotoa  mlio  wa  kuashirikia  kutokea  kwa  msiba,  mchawi na  yeye  hupiga  mluzi ima  kwa  mdogo ima  kwa  filimbi  ya  kichawi  kumjibu  bundi, na  bundi  asipo  jibu  mlio  huo, basi  mchawi  anakuwa  amejua  kuwa  siku  zake  zap  kuishi  hapa  duniani  zimefika  ukingoni.

Mtoto  anapozaliwa, wachawi  kwa  kutumia  uchawi  na nguvu  za  kiroho zap  bundi  hupeleka jina  la  mtoto  huyo  ili  kujua  atakuwa  nani  baadae, na  endapo  itajulikana  kwamba  mtoto  huyo  atakuwa  mtu  mkubwa  mwenye  mafanikio, basi  nyota  yake  itaibwa  mara  moja.
Nyota  hii inapochukuliwa  ima, huuzwa  kwa  mtu, hutumikishwa  msukule, ama  kuzikwa.
 
Nyota ya  mtoto  mchanga  inapo chukuliwa, hubadilishwa  na  nyota  chafu  na  matokeo  yake  mtoto  huyu  anaanza  kuishi  maisha  ambayo  si  yake.
Vile vile  kwa  kumtumia  bundi, wachawi  huweza  kurudisha  nyuma  jambo  baya  ambalo  lingemtokea  mtu  miaka  ya  mbeleni.
 
Kwa  mfano  ramani  yako  ya  maisha inaonyesha  kuwa  utafariki  kwa  maradhi ya  kisukari  ukiwa  na  miaka  75. Wachawi   kwa  kumtumia  bundi  wanaweza  kuyarejesha  nyuma  maradhi  hayo  na  kukufanya  uyapate  ukiwa  na  miaka thelathini.
 
Mambo  mengine  ya kichawi  ambayo  wachawi  huwatumia  bundi  kuyafanya  ni  pamoja  na :
1. Mavi  ya  bundi hutumika   kwenye  ungo wa  kusafiria  kichawi

2. Mavi  ya  bundi  huchanganywa  na  mavi  ya  chatu,  sokwe, nyani, maji ya maiti, mavi ya mtu  aliye  jisaidia akiwa  porini  pamoja  na  madawa mengine, katika kumtia  mtu  mikosi.

3. Matambiko  ya  biashara na  madini  migodini

4. Hutumika   kufungua  milango  ya  kuzimu  wakati wa  kuvuka  kutoka  duniani  kwenda  kuzima  kwa  njia  ya kupitia  baharini.

5. Kuwa  na  uwezo  wa  kuona  wachawi, kuona  mambo  yaliyo  jificha, mambo yatakayo  tokea  mbeleni, mambo  ya  siri.                                                                                       

6. Kuwakaribisha  watu   kwenye  malango   makuu  ya  kichawi,ya  miji, nchi  nakadhalika

Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )
© Copyright MZALENDO HURU
Back To Top