Ikiwa
vuguvugu la kuhama kwa wanasiasa limepamba moto nchini, Katibu wa
Itikadi na Uenezi Taifa wa ACT-Wazalendo, Ado Shaibu, amesema haoni hoja
ya msingi itakayo mshawishi kukihama chama hicho.
Ado
aliyasema hayo Novemba 9, 2017 siku moja baada ya aliyekuwa Mgombea
kiti cha Urais kwenye uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 kupitia ACT ambaye pia
alikuwa mwenyekiti wa chama hicho, Mama Anna Mgwira kuhamia CCM, uamuzi
alioutangaza kwenye Mkutano wa Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT)
uliofanyika mjini Dodoma.
Ado
alifunguka kuwa, katika kipindi cha wiki mbili zilizopita ambacho
hakuwepo kwenye mitandao ya kijamii na kupatikana kwenye simu
iliyozoeleka, kuna baadhi ya watu baada ya kurejea hewani, walimtumia
jumbe zenye kuhoji kama ameshahamia CCM kutoka ACT.
“Jibu
langu kwao lilikuwa jepesi. Siasa halisi si mzaha Kama mchezo wa
komborera. Kwamba Leo ujifiche hapa kesho pale Kisha ubutue. Siasa ni
itikadi. Siasa ni falsafa. Siasa ni sera. Siasa ni hisia za watu
waliokuamini na kukuheshimu. Ukiheshimu Itikadi, falsafa, sera na hisia
za watu waliokuheshimu na kukutumaini ndani na nje ya chama, hauwezi
kuhama hovyo Kama wacheza komborera wanavyobadili maficho yao,” alisema
na kuongeza.
“Kuhama
Chama ni lazima kusukumwe na hoja za msingi na zenye mashiko. Kwa sasa,
sijaona hoja yoyote ya maana ya kunifanya niondoke Act Wazalendo.”
Siku
za hivi karibuni kumekuwepo na wimbi kubwa la wanasiasa wa vyama vya
upinzani kuhamia chama Tawala CCM kwa madai ya kumuunga mkono Rais John
Magufuli kutokana na kuridhishwa na utendaji kazi wake, miongoni mwao
wapo waliokuwepo Wabunge, madiwani, viongozi kwenye vyama vya upinzani
na wanasiasa mashuhuli.
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )