Waziri Kivuli wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Godbless Lema amempongeza Rais John Magufuli kwa kutoa msamaha kwa wafungwa.
Pia, amemshauri kuwaangalia mahabusu waliokaa muda mrefu gerezani pasipo kupata haki.
Katika
maadhimisho ya uhuru wa Tanganyika (Tanzania Bara) Jumamosi Desemba
9,2017mkoani Dodoma, Rais Magufuli alitoa msamaha kwa wafungwa 8,157
kati yao 1,828 waliachiwa huru kuanzia siku hiyo.
Rais
John Magufuli jana Jumapili Desemba 10,2017 ametia saini nyaraka za
msamaha alioutoa kwa wafungwa 61 waliohukumiwa kunyongwa hadi kufa na
wawili Nguza Viking na Johnson Nguza (Papii Kocha) waliohukumiwa kifungo
cha maisha jela.
Msamaha huo umeonekana kumgusa Lema ambaye ni Waziri Kivuli wa Mambo ya Ndani ya Nchi. Lema amesema kuna mateso wanayopata mahabusu ambayo yanahitaji kuangaliwa.
“Rais
Magufuli, Mungu akubariki kwa msamaha uliotoa jana kwa wafungwa na hasa
wale waliokaa magereza muda mrefu pamoja na wazee, msamaha ni ibada,”
amesema Lema ambaye pia ni mbunge wa Arusha Mjini (Chadema).
“Ni
msamaha muhimu kwao, mtu aliyehukumiwa maisha au kifo akipata msamaha
ni jambo jema sana, ninafurahi wamesamehewa sasa hawatakuwa tena
magereza maisha yao yote,”
“Nimefurahi
kwamba hata wale waliokuwa wamehukumiwa kunyongwa hasa wazee pia
wamepata msamaha, kwangu ninaona ni jambo jema na zuri, kwa mtu anayejua
huzuni ya magereza atakubaliana nami.”
Kuhusu mahabusu, Lema amesema, ‘’Wako mahabusu wamekuwa magereza kwa muda mrefu bila kesi zao kukamilika. Mheshimiwa Rais fuatilia watu kama hawa pia.”
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )