Upande
wa Jamhuri umewasilisha hati ya kiapo kuzuia dhamana ya washtakiwa
wanne wanaokabiliwa na kesi ya kujihusisha na vitendo vinavyoashiria
mapenzi ya jinsia moja na makosa ya kimtandano katika Mahakama ya Hakimu
Mkazi Mwanza.
Hati hiyo imewasilishwa mahakamani leo Jumatano Desemba 13,2017 na Wakili wa Serikali, Emmanuel Luvinga.
Washtakiwa
katika shauri hilo namba 548/2017 ni Milembe Suleiman na Janeth Sonza,
mwanafunzi wa sheria katika Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino jijini
Mwanza, wanadaiwa kuvishana pete ya uchumba licha ya wote wawili kuwa
wanawake.
Wengine
ni Aneth Mukuki anayeshtakiwa kwa kufanikisha sherehe za wawili hao
kuvishana pete na Richard Fabian anayekabiliwa na shtaka la kusambaza
picha za tukio hilo mitandaoni.
Mbele
ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Mfawidhi, Wilbert Chuma anayesikiliza shauri
hilo, mawakili wa utetezi wameomba muda wa kuipitia na kuijibu hati
hiyo kwa hati kinzani kwa sababu hawakuwa wameipata kabla ya
kuwasilishwa mahakamani.
Ombi hilo lilikubaliwa na Mahakama ambayo imeahirisha shauri hilo kwa muda.
Mawakili wa utetezi ni Ogastin Kulwa, Mashaka Tuguta na Jebra Kimbole.
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )