Mkuu
wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP), Simon Sirro amefunguka na kuwataka
watu wanaofikiria kutaka uharifu waache mara moja kwani wasipofanya
hivyo wanaweza kujikuta wameishia gerezani au kukatishwa uhai wao na
wakashindwa kusherehekea sikukuu.
Simon Sirro ametoa kauli hiyo mkoani Lindi, alipokuwa anazungumza na waandishi wa vyombo mbalimbali vya Habari.
Kamanda
Sirro amesema mtu yeyote anayefikiria kufanya vurugu au vitendo vya
uhalifu wa namna mbalimbali,ikiwemo wa kutumia siraha ni vema akaacha,
vinginevyo anaweza akaishia gerezani au kupoteza maisha kabla ya hata
hajashehelekea sikukuu hizo.
"Nasema
tumejipanga vyema karibu timu zetu zote, zikiwemo za upelelezi, za
kiinterijensia na timu zetu za operesheni nazo zimejipanga kwa ajili ya
doria zikiwemo za helkopta, majini kila mahali kuhakikisha watanzania
wanaishi kwa amani na utulivu ndani ya Taifa lao" Alisema Sirro.
Aidha
Sirro alisema kuwepo kwa amani na utulivu kutawafanya wananchi
mbalimbali, wakiwemo wafanyabiashara kutekeleza majukumu yao vizuri
katika kujiletea maendeleo ndani ya nchi yao.
Mbali
na hilo IGP Sirro, ameonya kwa kusema wale wanaofikiria kutumia silaha
waachane na mpango huo mara moja , kwa kuwa ni vigumu kumkamata mtu
aliye na silaha na hivyo kitakachotokea ni ama mmojawapo kukatishwa uhai
wake, huku akiwataka waalifu kujiuliza mara mbili kabla ya kuchukuwa
silaha kwa lengo la kufanya uhalifu.
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )