Waziri wa ulinzi wa Tanzania Hussein Mwinyi akipokea maelezo katika kambi ya MONUSCO Beni
Waziri
wa ulinzi wa Tanzania, Hussein Mwinyi ametoa wito wa kudumisha
ushirikiano kati ya pande zote zinazo shiriki katika kuleta amani
mashariki ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).
Mwinyi
alitoa wito huo siku ya Ijuma alipowatembelea wanajeshi wa Tanzania
wanaoshiriki katika kikosi cha kimataifa cha kulinda amani mashariki ya
Congo, na kuwatembelea wanajeshi waliojeruhiwa wakati wa shambulizi la
Disemba 7, 2017.
Wanajeshi
14 wa Tanzania wa kikosi maalum cha nchi za Kusini mwa Afrika SADC
waliuwawa na wengine 44 kujeruhiwa walipo shambuliwa na waasi
wasiojulikana hadi hii leo katika kambi yao huko Semulik, karibu na mji
wa Beni.
Akizungumza
na waandishi wa habari kwenye uwanja wa ndege wa Beni, Waziri Mwinyi
alisema amefika kuwapa pole wanajeshi wa Tanzania na kuwatembelea
walojeruhiwa pamoja na kuwapa moyo kuendelea na jukumu lao la kurudisha
amani katika eneo la mashariki ya Kongo.
Akizungumzia
uchunguzi unaoendelea kuhusu shamblizi hilo, Mwinyi amesema hadi sasa
hawana habari zaidi, "sasa hivi ni mapema sana kusema fulani amefanya
hivi. Hatuna uhakika, UN pia haina uhakika na ndiyo maana tunasema ni
lazima uchunguzi ufanyike."
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )