Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli na
Mkewe Mhe. Mama Janeth Magufuli leo tarehe 17 Desemba, 2017 wameungana
na waumini wa Kanisa Kuu la Mtakatifu Paulo wa Msalaba, Jimbo Kuu
Katoliki la Dodoma kusali ibada ya Jumapili.
Akizungumza
baada ya Ibada hiyo Mhe. Rais Magufuli amewashukuru viongozi wote wa
dini na waumini wa madhehebu mbalimbali ya dini kwa kuendelea kuliombea
Taifa ili lidumishe amani na upendo.
Mhe.
Rais Magufuli amesema Serikali anayoiongoza inatambua juhudi
zinazofanywa na viongozi wa Dini katika kudumisha amani na upendo na
ameahidi kuwa itaendelea kushirikiana nao katika kujenga Tanzania bora.
“Nawaomba
viongozi wa madhehebu yote ya dini tuendelee kuliombea Taifa letu liwe
na amani na upendo, na Serikali itashirikiana nanyi muda wote” amesema
Mhe. Rais Magufuli.
Padre
wa kanisa hilo Fr. Sergio Madinda amemshukuru Mhe. Rais kwa ushirikiano
wake na kanisa na pia amemshukuru kwa uamuzi wake wa kuhamishia
Serikali Dodoma.
Katika
Ibada hiyo Mhe. Rais Magufuli ametoa Shilingi Milioni 3 kwa ajili ya
kuchangia ujenzi wa Kigango cha Michese na kwaya ya Kanisa Kuu la
Mtakatifu Paulo wa Msalaba.
Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dodoma
17 Desemba, 2017
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )