Baadhi ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) wameingia hofu baada ya mabweni wanayoishi kuwa na nyufa.
Mabweni hayo yanayotumiwa na wavulana katika jengo la Block A yana nyufa sehemu mbalimbali kuanzia chini hadi ghorofa ya tatu.
Mbunge wa serikali ya wanafunzi (Daruso), Simon Masenga amesema nyufa hizo zilianza kuonekana wiki mbili zilizopita.
Amesema
walitoa taarifa kwa meneja wa hosteli lakini majibu waliyopewa ni kuwa
majengo hayo yako chini ya Wakala wa Majengo Tanzania (TBA).
Mbunge
mwingine wa serikali ya wanafunzi, Kumbusho Dawson amesema leo Jumatatu
Desemba 4,2017 kuwa majengo hayo yana upungufu, ukiwemo wa maji kutuama
kwenye bafu na kutokuwa na makabati.
"Tumelalamika
kwa meneja wa mabweni kuhusu upungufu katika majengo haya na majibu
tunayopewa ni kuwa bado yako chini ya TBA," amesema Dawson.
Majengo hayo yaliyojengwa na TBA kwa miezi minane yakielezwa kugharimu Sh10 bilioni yalizinduliwa Aprili 15,2017.
Ujenzi ulifanyika ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Rais John Magufuli la kumaliza tatizo la malazi kwa wanafunzi wa UDSM.
Picha zinazoonyesha nyufa kwenye majengo hayo zilianza kusambaa mitandaoni jana Jumapili Desemba 3,2017.
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )