Muigizaji
wa filamu bongo ambaye sasa anajihusisha zaidi na ujasiriamali,
Jackline Wolper, amesema anapenda wanaume wenye maumbile madogo kwani
yeye mwenyewe maumbile yake ni madogo.
Akizungumza
kwenye kipindi cha Friday Night Live cha EATV Jackline Wolper amesema
hana sababu ya kupenda au kusifia wanaume wenye maumbile makubwa wakati
yeye maumbile yake ni madogo.
"Actualy
siwezi kusema nachukuliaje wanaume wenye maumbile madogo, na ndio
nawapenda pia, kwa sababu mimi mwenyewe mdogo, nitapendaje vitu vikubwa
ambavyo siwezi kuvihimili?
"Unajua
mwanamke anayesema mwanaume mashine namshangaa, mwanaume pesa bwana,
mwanamke ambaye anajua maisha, hawezi kusema mwanaume mashine, mimi
mwenyewe siwezi kusifia mashine", amesema Wolper.
Pamoja
na hayo Jackline Wolpler amesema kwa sasa hataki kujihusisha sana na
masuala ya mahusiano, kwani amezipa kipaumbele kazi zake tu.
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )