Featured
Loading...

Kuongea Kiingereza ni Kipaji – Shilole Afunguka


Msanii wa muziki, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ amefunguka kwa kudai kuongea Kiingereza siyo kitu cha mchezo kama watu wanavyofikiria.

Akizungumza katika kipindi cha Enewz cha East Africa Television Jumatano hii, Shilole alisema yeye amepigana mpaka ameweza kuongea Kiingereza.

“Kiingereza ni kipaji jamani, mimi naongea Kiingereza wakati ambao najisikia. Lakini asikwambie mtu, kuongea Kiingereza ni kipaji,” alisema Shilole.

Muimbaji huyo ameachia kazi mpya iitwayo ‘Say My Name.’

Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )
© Copyright MZALENDO HURU
Back To Top