Mei 8 2016
ni siku ya wakinamama Duniani, Tanzania pia imekuwa moja ya nchi
iliyofanya maadhimisho hayo, Hapa nakukutanisha na Makamu wa Rais Samia Suluhu ambaye leo alikuwa Dodoma na baada ya kuhutubia wananchi wake akaguswa na hili la kodi kwa wafanyabiashara wanawake na kutoa maamuzi..
‘Mimi
kama mama nachukizwa na jambo moja kubwa nililoliona kule Moshi na
baaadhi ya maeneo kule Arusha, kuna kodi zinatolewa katika masoko,
Ukipita masoko ya Moshi na Arusha Unakuta wakinamama wanasimama na ndizi
kichwani anasimama na ndizi yake hadi aiuze’
‘Na akiiweka chini anatozwa kodi na kodi ile ni sawa na bei anayoiuza. Kwahiyo mama anabakia na ndizi yake kichwni mpaka aiuze.’
‘Naelekeza
Wakurugenzi wa halmashauri kufuta kodi hiyo mara moja, na nitafanya
ziara ya kufuatilia utekelezaji wa jambo hili. Na siotu kodi za ndizi
bali kodi zote zinazowazalilissha wakinamama’
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )