Featured
Loading...

HAYA NDIYO MAMBO MAKUU 5 YALIYOSABABISHA GOODLUCK JONATHAN KUSHINDWA


Taifa la Nigeria jana liliingia katika historia mpya baada ya kushuhudiwa chama cha upinzani kikishinda katika uchaguzi mkuu wa nchi hiyo pale Jenarali Muhammadou Buhari wa chama pinzani cha All Progressive Congress (APC) alipomshinda mpinzani wake aliekuwa rais wa nchi hiyo na kilichokuwa  chama tawala cha People's Democratic Party (PDP)  Goodluck Jonathan  


Rais aliyekuwa  madarakani Goodluck Jonathan amesalia akijutia maamuzi yake baada ya raia wa taifa hilo kubwa zaidi Afrika kiuchumi kumpigia kura mpinzani wake mkuu Muhammadu Buhari .



Haya  hapa ni mambo makuu 5 ambayo  yanaelezea  kwanini raia wa Nigeria walimng'oa Goodluck Jonathan madarakani
. 1: Haikuwa rahisi kuiba kura
Katika Uchaguzi uliopita wa  mwaka wa 2007 ,tuhuma za wizi wa kura za urais ziliibuka huku wadadisi na wachunguzi  wakisema waziwazikuwa kura hazikuwa za huru wala haki.
Ripoti ya wachunguzi  katika uchaguzi wa mwaka wa 2011 ilisema kuwa haukuwa wa uhuru japo ilisema kuwa idadi ya wizi ilikuwa imepungua mno.
Kufuatia ripoti hiyo tume huru ya uchaguzi nchini humo ilijiandaa na kuziba mianya iliyokuwa imebainika.
Tume hiyo ilinunua mashine za kuwasajili wapiga kura kwa njia ya kielektroniki na ving'amuzi vilivyotumika kubaini data ya mpiga kura.
Chama cha rais Goodluck Jonathan People's Democratic Party (PDP) kilikuwa kimepoteza ufuasi mkubwa katika majimbo yaliyokuwa ngome yake.

2 Boko Haram
Uchaguzi huo umetangazwa huku raia wengi wa Nigeria wakikabiliwa na changamoto ya usalama wao haswa wakiwa mijini.
Hii inafwatia tishio la kundi la wapiganaji wa kiislamu wa Boko Haram ambao walikuwa wanaonekana ni kama wameishinda maarifa vyombo vya usalama vya nchi hiyo
Boko Haram iliwaua zaidi ya watu elfu 20 na kuwalazimisha wenyeji zaidi ya milioni tatu kutoroka makwao.
Rais Jonathan hakuwa na jibu dhidi yao na alionekana mnyonge hadi majuzi majeshi ya muungano wa mataifa jirani yaliposhirikiana na jeshi la Nigeria na kuwavamia wanamgambo hao wa kiislamu.

. 3 Muungano wa Upinzani
Chama cha PDP kiliundwa kwa muungano wa viongozi kutoka matabaka ya kaskazini na vilevile kusini mwa taifa hilo.
Hata hivyo kufuatia udhaifu  wa rais Jonathan viongozi wengi waliokuwa nguzo ya umoja huo walitawanyika.
Muungano wa viongozi wa upinzani chini ya nembo ya chama cha All Progressives Congress (APC)kuliwasaidia kukusanya kura zote katika kapu moja.


4 Uchumi mkubwa zaidi Afrika
Ijapokuwa Nigeria inasifika kuwa taifa kubwa zaidi barani Afrika kiuchumi ,ukiwauliza raia wa Nigeria iwapo wamenufaika kwa njia yeyote ile watakuambia kuwa hawajanufaika kwa hali yeyote ile.
Takriban nusu ya raia wa nigeria wanaishi kwa hali duni ya uchochole na umaskini.
Wengi wao wanalaumu ufisadi wa viongozi na ubadhirifu wa mali ya umma.
Uchumi wa Nigeria umekuwa kwa kiwango cha asilimia 5% kwa mwaka kutokana na mauzo ya mafuta lakini raia wengi hawakutaka kuendelea na utawala wa Goodluck.
Takwimu zinaonyesha kuwa kila watu 10 wanaohitimu chuo kikuu nchini Nigeria 6 kati yao wanakuwa hawana ajira

5 Ni wakati wa Mabadiliko
Wafuasi wa chama cha upinzani APC walichagua kibwagizo chao kikuu kuwa ''Mabadiliko''.
Na huenda wanigeria hawakuwa wanataka kuendelea na hali ilivyokuwa wakati huu.
PDP imekuwa madarakani tangu mwaka wa 1999, utawala wa kiimla ulipomalizika.
Mwaka huu 2015 Wapiga kura wameamua kumchagua kiongozi atakayekuwa na msimamo thabiti na uwezo wa kukabiliana na matatizo mengi yanayowasakama
Hata hivyo kinachosubiriwa na wengi ni kuona iwapo rais Buhari ataleta mabadiliko kweli alivyowaagiza wapiga kura.

Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )
© Copyright MZALENDO HURU
Back To Top