Waliozoea kusafiri kwa mabasi kwa siku moja kutoka Dar es salaam kwenda
Mbeya na kutoka Dar es salaam kwenda Mwanza na kwingineko kwenye umbali
sawa na huo, sasa inabidi wajipange kisaikolojia kutumia siku mbili
kukamilisha safari hizo. Hayo yamebainishwa na Meneja Usalama Barabarani
na Mazingira wa SUMATRA, Geofrey Silanda. Uamuzi huo umetokana na
utafiti uliofanywa na mamlaka hiyo na kubaini kwamba mabasi yanayofanya
safari kwenye mikoa hiyo hayapaswi kusafiri kwa siku moja.
Toa maoni yako
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )