Featured
Loading...

RIWAYA: Sorry Madam - Sehemu ya 49 & 50 (Riwaya inawafaa kuanzia miaka 18 na kuendelea )


 
Mtunzi : Eddazaria g.Msulwa


Ilipoishia....
Nikaachia msunyo mkali na kuirudiisha gari yangu upande wa kushoto nilipo toka na jamaa akanifwata nilipo,sikuwa na budi zaidi ya kutoka nje ya barabara kuepika kugongana uso kwa uso na gari hilo.Gari ikaanza kunishinda nguvu badala ya kufunga breki kwa kuchangunyikiwa nikawa na kazi ya kuongeza kasi.Nikastukia gari ikaanza kupiaga kubingiria kwa kasi ya ajaba.Jinsi inavyobingiria ndivyo jinsi ninavyo jigonga ndani ya gari hadi giza jingi likayavaa macho yangu na kutulia kimya...

Endelea...
....Kwa mbali nikaanza kusikia milio ya ndege,nikajaribu kuyafumbua macho yangu ila kichwa changu nikakuta kinaniuma sana.Nikakajikaza sana na kuyafumbua macho yangu yakakutana na mwanga mkali  wa juu unao ingi kwenye kioo cha mbele cha gari langu.Nikajaribu kujichunguza kwa umakini na kugundua mikono yangu imefungwa pamoja na mskani wa gari langu.Kila nanapovuta taswira ya sehemu nilipo,sijawahi kuiona siku hata moja.Miti mirefu iliyopo kwenye eneo zima lililo gari langu likazidia kunichanganya.

Baada ya muda kiogo nikastukia mlango ukifunguliwa na akasimama jamaa mwenye bunduki mbele yangu,huku akiwa amevalia mavazi meusi kuanzia juu hasi chini.Akanitazama kwa umakini kisha akaifungua mikono yangu na kunitoa ndani ya gari na kunitupa chini.Akaninyanyua na kuniweka begani,tukaanza kuondoka pasipo kuwezakujua ni wapi tunapo elekea,hatua kadhaa mbele nikaona jumba kubwa lililo zungukwa na miti mingi ambayo kwa mbali huwezi kugundua kama kuna jumba kubwa kama hili

Tukaingia ndani na jamaa akanibwa mbele ya watu wapatao ishirini walio shika bunduki zao.Mapigo ya moyo yakaanza kunienda kasi baada ya macho yangu kutazamana na mzee godwin ambaya jicho lake moja ameliziba na kitambaa cheusi.Mzee godwin akatabasamua na kumuamuru mtu aliye nilete katika sehemu hii kunifungua mikono yangu.
“eddy.....Eddy......Eddy my x-son”

Mzee godwin alizungumza kwa dharau kubwa huku akinizunguaka taratibu katika sehmu ambayo nimesimama.Kila niliye jaribu kumtazama sura yake haikuonyesha huruma hata kidogo japo kuna wasichana watatu ila nao sura zao zinaonekana zimejaa ukatili mkubwa.Kitu mabacho kinaniumiza
“usishangae sana kwa maana vita yangu mimi na wewe bado inaendelea”

Kwa haraka ninakumbuka kwamba huyu mzee niliambiwa kuwa amechanganyikiwa sasa sijajua imekuwaje hadi leo anamiliki kundi kubwa la watu kiasi hichi,gafla mzee godwin akanipiga mtama ulio niangusha chini vibaya sana na kunifanya niaanze kutoa miguno ya maumivu

“wewe ndio,chanzo cha kuipoteza mali yangu.Wewe ndio mtu uliye mteka mwangua.Wewe sio mwanangu niambie yupo wapi mwanangu?”
Maswali ya mzee godwin yanakizidi kunichanganya kwani sikujua mwanaye anaye mzungumzia ambaye anadai nimemteka ni nani

“mi...Mi mbona sikuelewi?”
“ahaa hunielewi?”
Mzee godwin akanipiga teke la kifua na kunifanya nijikunje huku maumivu yakizidi kunitawala kwenye kifua changu.Machozi mengi yakaendelea kunitoka
“ninakwenda kumuua mama yako?”

“hapana baba.Kumbuka kuwa mama ni mke wako wa ndoa.Mtu wa kuniua ni mimi hapa na wala si mama yangu.Nipo chini ya miguu yako”
Nilizungumaza huku nikiwa nimeishika miguu ya mzee godwin,akarudi nyuma na kunipiga teke lililo ifanya mikono yangu kuuiachia miguu yake

“yupo wapi,manka mwanangu?”
“manka,yupo arusha”
“arusha,arusha.Ndipo ulip kwenda kumficha si ndio?”
“hapana baba,mbona manka yeye ndio aliye watoroka nyinyi?”
“mimi sio baba yako na manka mwangu hawezi kunikimbia mimi”

Mzee godwin alizungumza kwa hasira huku akinitazama,akamuomba mwenzake mmoja waya wa umeme ambao unene wake  ni 1.5,akaukunja mara mbili na kuanza kunichapa nao kwa fujo huku akinitukana mimi na mama yangu.Nikazidi kulia kwa uchungu mkubwa,maumivu mengi yakazidi kuusonga mwili wangu.
Kila ninapojaribu kuizuia sehemu moja ya mwili wangu isichape basi sehemu nyingine ni lazima ichapwe kwa waya huu.Mzee godwin bila ya huruma akachukua pakti mbili zenye unga mwekundu na kuanza kunimwagia mwilini mwangu,hapa ndipo nikagunda ni unga wa pilipili ndio anao nimwagia.

Mauimivu ninayo yapata hayana mfano,kikubwa ambacho ninakilinda ni macho yangu yasiingie pilipili hii.Mzee godwin akawaamrisha watu wake wakamtafute manka na kumleta hapa mara moja.Mimi wakaniburura na kuniingiaza kwenye chumba kimoja ambacho kina giza nene.Baada ya dakika kama mbili nikastukia taa tatu kubwa zikiwaka zenye mwanga mkali ambao ukaanza kuniungaza mwili wangu,jasho ambalo linanimwagika kutokana na mwanga mkali,likazidi kunichoma kwenye vidonda vyangu.
Sehemu zote za majeraha ya mwili wangu,zikazidi kuniuma kiasi kwamba maumivu makali yakazidi kunitwala.Taa zikaendelea kuwa zaidi ya dakika kama kumi kisha zikazimwa.Nikabaki nikiwa nimekaa chini nimejikinyata mwili mzima huku nikiwa ninatetemeka kma nimepigwa na shoti.

Nikaendelea kukaa ndani ya chumba kwa muda mrefu,sikujua jinsi masaa yanavyo kwenda,mlango ukafunguliwa na ikawasha taa ya kawaida,mbele yangu akasimama mwanamke mrefu mwenye mwili mmnene kiasi.Mikononi akiwa ameshika sahani yenye chakua kingi,akachuchumaa na kuniwekea

“kama unaweza kula sawa,kama hutoweza kula acha”
Alizungumza na kutoka ndani ya chumba na kukifunga,nikaivuta sahani yenye chakula taratibu.Nikaanza kula wali uliopikwa vibaya kwani wala haukuiva vizuri,sikuwa na jinsi zaidi ya kuendelea kuula huku nikiwa nimejikaza.Mwili mzima unanitetemeka kwa maumivu makali,chakula kingi kinamwagika chini kutokana na mikono yangu kutetemeka sana kiasi kwamba hata kukishika chakula ninashindwa.Sikumaliza kukila chakula kutokana na kutetemeka sana mwili wangu,

Masaa yakazidi kwenda pasipo kujua nini muafaka wangu wa kukaa ndani ya hili jumba.Nikaanza kukichunguza chumba sehemu yote na kugundua kimefungwa taa nyingi zenye ukubwa mbali mbali,nyengine zinaukubwa kama taa zinazo fungwa kwenye viwanja vya mpira ndio maana zina mwanga mkali sana.
Nikauchunguza mwili wangu na sehemu kubwa imeujeruhiwa.Nikiwa nimesimama nikastukia mlango ukifunguliwa,nikakaa kwa muda ila sikuona mtu akiingia ndani ya chumba.Taratibu nikaanza kupiga hatua za kwenda nje,nikachungulia wala sikumuona mtu wa aina yoyote.Nikapiga  hatu na kwenda nje kabisa na sikuona mtu wa aina yoyote katika eneo hili

Nikazidi kwenda mbele na yumba nzima inavyumba vingi sana,nikaendelea kuchunguza hadi nikafika sebleni.Nikachungulia dirishani na kumuona mzee godwin akiwa amesimama na watu wake wakilitazama gari linalo simama,baada ya gari kusimama wakashuka watu wawili walio valia mavazi meusi kish mmoja akafungua mlango wa nyuma akashuka manka akiwa na madam mery.Mzee godwin akamkumatia manka kwa furaha ila manka hakuonekana kuwa na furaha ya aina yoyote

“mama yangu mbona huna furaha?”
“baba kwa nini siku zote ulinificha?”
“nilikuficha na nini mwanangu?”
“baba kumbe eddy ni ndugu yangu.Umecha hadi nimefanya naye vitendo vya ajabu nikidhani ni mtu wa kaiwada kama wengine”
Maneno ya manka yakaibadilisha kabisa sura ya mzee godwin,akikunja kana kwamba amepigwa na mshale wa mgongo
“ina maana eddy amekubaka?”

“sio amenibaka,eddy alikuwa ni mpenzi wangu na hadi amenipatia ujauzito ila kwa bahati mbaya mimba ikatoka”
Mzee godwin akajishika kichwa na kuzunguka mara mbili huku akisunya misunyo mkali

“nitamuua eddy leo mbele yako”
Mzee godwin alizunguza na kuanza kupiga hatua za kuingilia kwenye mlango wa sebleni.Kabla sijafanya kitu chochote nikastukia nikishikwa kwa nyuma na kuzibwa mdomo
“shiii”

Ilikuwa ni sauti ya kike,mwanamke aliye nishika kwa nyuma akaanza kunivuta kwa nyuma huku tukielekea gizani.Tukatokea upande wa pili wa nyumba kwenye miti mingi,ndipo nikagundua mtu aliye nishika ni yule dada aliyekuwa ameniletea chakula

“kimbia kabla kifo hakija kukuta hapa”
Msichana alizungumza,huku akiwa amenitazama kwa macho makali,
“asante”
“amina ninaitwa”
“eddy”
“ninakujua,haya nenda”

Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )
© Copyright MZALENDO HURU
Back To Top