Featured
Loading...

Simba, Azam Hapatoshi.. Warushiana Tambo Mechi ya Leo Ligi Kuu Bara


Michuano ya Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara inatarajia kuendelea tena leo ambapo Simba na Azam FC zinazotarajia kukutana kwenye Uwanja wa Uhuru zimeelezea kuhusu mchezo huo.

Afisa Habari wa Simba SC Haji Manara amesema, kikosi kimejiandaa vizuri kwa ajili ya kuweza kupambana na wanauchukulia huo kama michezo mingine hivyo wanaamini wataweza kuvuna pointi tatu mbele ya Azam FC.

Manara amesema, mpaka sasa wana majeruhi wawili pekee ambao ni mshambuliaji Ibrahim Ajibu na kiungo Mwinyi Kazimoto ambao daktari anaendelea kuangalia hali zao kama wataweza kucheza mchezo wa kesho au bado wataendelea kuwa katika uangalizi.

Kwa upande wake Afisa Habari wa Azam FC Jafary Iddy Maganga amesema, mchezo huo utakuwa na changamoto kubwa kutokana na wote kuwa na pointi sawa katika msimamo wa ligi lakini watapambana ili kuhakikisha wanashinda huku akiwataka waamuzi wa mchezo huo kusimamia sheria 17 za soka ili kuhakikisha timu inashinda kutokana na uwezo wake.

Maganga amesema, kwa upande wao majeruhi ni walewale ambao walikuwa nao katika mchezo dhidi ya Mbeya City ambao ni mshambuliaji Gonazo Bi Thomas, Beki Erasto Nyoni na Agrey Morris pamoja na Mlinzi wa kati Paschal Wawa.

Michezo mingine itakayopigwa hapo kesho ni Mtibwa Sugar wakiwakaribisha Kagera Sugar Uwanja wa Manungu Mkoani Morogoro, Mbeya City akiwakaribisha Tanzania Prisons Uwanja wa Sokoine Mkoani Mbeya, Mwadui FC akiikaribisha Yanga Uwanja wa Mwadui Mjini Shinyanga na Ruvu Shooting akiikaribisha Mbao FC Uwanja wa Mabatini Mkoani Pwani

Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )
© Copyright MZALENDO HURU
Back To Top