Featured
Loading...

Ebwana Weee!! Umesikia Alichokisema Said Fella Juu ya Mziki wa Taarabu na Mipango ya Kundi Lake la Yah TMK Taarab?


 
Meneja ambaye amejizolea umaarufu mkubwa kutokana na mchango wake wa kuinua vipaji vya wanamuziki wachanga hadi kuwa maarufu, Saidi Fella ‘Mkubwa Fella’ amedai muziki wa taarab haujakufa kama baadhi ya watu wanavyodai.
Mkurugenzi huyo wa Yamoto Band ambaye ameingia kwenye muziki wa taarab kwa kuanzisha bendi ya ‘Yah TMK Taarab’ amedai hakuna ukweli wowote kwamba muziki wa taarab umekufa.
“Mimi siamini kwamba muziki wa taarab umekufa, mashabiki wapo wanazaliwa kila siku wanataka muziki mzuri,” Mkubwa Fella alikiambia kipindi cha Jahazi ya Sham Shama ya ITV.
Fella amesema yeye pamoja na bendi yake hiyo wamejipanga kuleta ushindani mpya kwenye muziki wa bendi kwa kuachia kazi nzuri.
“Ukija kwenye Yah TMK Taarab utapata kila kitu, sasa hivi tupo chimbo tunaanda kazi nzuri, kwa sababu ingawa tuna watu ambao wanamajina makubwa au wana uwezo mkubwa lakini mashabiki hawataki majina, wanataka kazi, kwahiyo sisi tumejipanga vizuri na tunakuja kutoa burudani kwa sababu mashabiki wapo wengi wanataka kazi,” alisema Fella.

Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )
© Copyright MZALENDO HURU
Back To Top